-
Shangilieni Pamoja na Mungu Mwenye FurahaMnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
-
-
6, 7. Ni mambo gani yaliyomsaidia Yesu kudumisha shangwe?
6 Namna gani Yesu—yeye alidumishaje shangwe yake? Akiwa kiumbe wa roho mwenye nguvu huko mbinguni, Yesu alikuwa na fursa ya kutazama matendo ya wanaume na wanawake duniani. Hali yao ya kutokuwa wakamilifu ilikuwa wazi, hata hivyo Yesu aliwapenda. (Mithali 8:31) Baadaye, alipokuja duniani na “[ku]kaa miongoni” mwa wanadamu, hakubadili maoni yake kuelekea wanadamu. (Yohana 1:14) Ni nini kilichomwezesha Mwana mkamilifu wa Mungu adumishe mtazamo huo mzuri kuelekea wanadamu wenye dhambi?
7 Kwanza kabisa, Yesu alikuwa na maoni ya kiasi kujihusu na kuhusu wengine. Alijua kwamba hangeweza kugeuza imani ya watu wote ulimwenguni. (Mathayo 10:32-39) Kwa hiyo alishangilia hata kama ni mtu mmoja tu mnyofu aliyekubali ujumbe wa Ufalme. Ingawa wakati fulani mwenendo na mtazamo wa wanafunzi wake haukupendeza, Yesu alijua kwamba walitaka kufanya mapenzi ya Mungu kutoka moyoni, na aliwapenda kwa sababu hiyo. (Luka 9:46; 22:24, 28-32, 60-62) Katika sala aliyomtolea Baba yake wa kimbingu, twaweza kuona kwamba Yesu alitaja jinsi wanafunzi wake walivyojiendesha ifaavyo kufikia wakati huo: “Nao wameshika neno lako.”—Yohana 17:6.
-
-
Shangilieni Pamoja na Mungu Mwenye FurahaMnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
-
-
Je, twaweza kufuata kwa ukaribu zaidi hatua za Yesu kwa kudumisha mtazamo unaofaa kuelekea hali zetu za sasa, na vilevile kuwa wenye kiasi katika mambo tunayotarajia kutoka kwetu na kwa wengine?
-