-
Je, Kweli Mungu Anawajali Wanawake?Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 1
-
-
Hata hivyo, kuanzia karne ya nne K.W.K., dini ya Kiyahudi ilianza kuiga tamaduni za Wagiriki, ambao waliwaona wanawake kuwa duni.—Ona sanduku lenye kichwa “Ubaguzi Dhidi ya Wanawake Katika Maandishi ya Kale.”
Kwa mfano, mtunga-mashairi Mgiriki Hesiod (aliyeishi karne ya nane K.W.K.) aliwalaumu wanawake kwa sababu ya matatizo yote yanayowapata wanadamu. Katika shairi lake linaloitwa Theogony, alizungumza kuhusu “jamii na kabila hatari la wanawake ambao wanaishi katikati ya wanaume na kuwasababishia matatizo mengi.” Wazo hilo liliingizwa katika dini ya Kiyahudi mwanzoni mwa karne ya pili K.W.K. Talmud, ambayo ilianza kuandikwa katika karne ya pili W.K. na kuendelea, iliwaonya wanaume hivi: “Msizungumze sana na wanawake, kwa sababu hilo litawaingiza katika upotovu wa maadili.”
-