-
Gamalieli—Alimfundisha Sauli wa TarsoMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
-
-
Gamalieli alikuwa Farisayo aliyejulikana sana. Alikuwa mjukuu wa kiume wa Hillel yule Mkubwa, aliyekuwa ameanzisha kimojapo vile vikundi vikubwa viwili vya kitheolojia katika Dini ya Kiyahudi ya Kifarisayo.a Njia ya kufundisha ya Hillel ilionwa kuwa yenye uvumilivu zaidi kuliko ile ya mshindani wake, Shammai. Baada ya uharibifu wa hekalu la Yerusalemu katika 70 W.K., Bet Hillel (Nyumba ya Hillel) ilipendwa kuliko Bet Shammai (Nyumba ya Shammai). Nyumba ya Hillel ikawa wonyesho halali wa Dini ya Kiyahudi, kwa kuwa mafarakano mengine yote yalipotelea mbali pamoja na uharibifu wa hekalu. Maamuzi ya Bet Hillel mara nyingi ndiyo msingi wa sheria ya Kiyahudi katika Mishnah, ambayo ikawa msingi wa Talmud, na yaonekana uvutano wa Gamalieli ulikuwa jambo hasa lililofanya imani hiyo iongoze.
Gamalieli aliheshimiwa sana hivi kwamba alikuwa wa kwanza kuitwa raban, jina la cheo la juu kuliko la rabi. Kwa kweli, Gamalieli akawa mtu mwenye kustahiwa sana hivi kwamba Mishnah yasema hivi juu yake: “Raban Gamalieli mkubwa alipokufa utukufu wa Torah uliisha, na utakato na utakatifu [kihalisi “mtengano”] ukaisha.”—Sotah 9:15.
-
-
Gamalieli—Alimfundisha Sauli wa TarsoMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
-
-
Ikiwa Paulo angaliendelea kuwa mwanafunzi wa Gamalieli, angalikuwa na cheo kikubwa. Wengine katika kikundi cha Gamalieli walisaidia katika kuamua wakati ujao wa Dini ya Kiyahudi. Kwa mfano, Simeoni, mwana wa Gamalieli, labda mwanafunzi pamoja na Paulo, alikuwa na fungu kubwa katika kuasi kwa Wayahudi dhidi ya Roma. Baada ya uharibifu wa hekalu, Gamalieli 2, mjukuu wa kiume wa Gamalieli, alirudisha mamlaka ya Sanhedrini, akiihamisha hadi Yavneh. Judah Ha-Nasi, mjukuu wa kiume wa Gamalieli 2, alikuwa mkusanyaji wa Mishnah, ambayo imekuwa jiwe la msingi la imani ya Kiyahudi kufikia siku yetu.
-