Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ole Wao Waasi!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • [Picha katika ukurasa wa 141]

      Yehova atawatoza hesabu wale wanaowaonea wengine

  • Ole Wao Waasi!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Waamuzi Wafisadi Wakabili Mwamuzi Wao

      17, 18. Mifumo ya kisheria na ya utawala ya Israeli ina ufisadi gani?

      17 Kisha Yehova akaza jicho lake lenye kuhukumu juu ya waamuzi wafisadi wa Israeli na maofisa wengine. Wao hutumia vibaya mamlaka yao kwa kuwapora maskini na waliotaabishwa ambao huwaendea ili kutafuta haki. Isaya asema: “Ole wao wawekao amri zisizo za haki, na waandishi waandikao maneno ya ushupavu; ili kumpotosha mhitaji asipate haki yake, na kuwanyang’anya maskini wa watu wangu haki yao; ili wajane wawe mateka yao, na kuwafanya yatima waliofiwa na baba zao kuwa mawindo yao!”—Isaya 10:1, 2.

      18 Sheria ya Yehova hukataza namna zote za ukosefu wa haki: “Msitende yasiyo haki katika hukumu, usimpendelee mtu maskini, wala kumstahi mwenye nguvu.” (Mambo ya Walawi 19:15) Maofisa hao waipuuza sheria hiyo, na kujiwekea “amri zisizo za haki” ili kuhalalisha wizi ulio wazi na wenye ukatili sana—kutwaa mali chache za wajane na mayatima. Kwa wazi, miungu vipofu ya Israeli haioni ukosefu huo wa haki, lakini Yehova auona. Kupitia Isaya, Yehova sasa awakazia fikira waamuzi hao waovu.

      19, 20. Hali ya waamuzi wafisadi wa Israeli itabadilishwaje, na “utukufu” wao utakuwaje?

      19 “Nanyi mtafanya nini siku ya kujiliwa, na wakati wa uangamivu, utakaokuja kutoka mbali sana? Je! mtamkimbilia nani mpate msaada? na utukufu wenu mtauacha wapi? Watainama chini ya wafungwa tu, wataanguka chini yao waliouawa.” (Isaya 10:3, 4a) Wajane na mayatima hawana waamuzi wenye haki wa kukata rufani kwao. Basi yastahili sana kwa kuwa Yehova sasa awauliza waamuzi hao Waisraeli wafisadi watamwendea nani kwa sababu sasa Yehova anataka watoe hesabu. Naam, karibuni watatambua kuwa “ni jambo lenye kuhofisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.”—Waebrania 10:31.

      20 “Utukufu” wa waamuzi hao waovu—fahari ya kilimwengu, staha, na uwezo unaotokana na mali na cheo chao—hautadumu. Baadhi yao watakuwa wafungwa wa vita, “watainama chini,” au kuchutama, kati ya wafungwa wengine, ilhali wengine nao watauawa, na maiti za waliokufa vitani zitafunika maiti zao. “Utukufu” wao watia ndani mali yao waliyopata kwa ufisadi, itakayoporwa na adui.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki