-
Jiji Kubwa LateketezwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
lakini katika 1918 Bwana Yehova na “mjumbe wa agano [la Kiabrahamu]” wake, Yesu Kristo, alianza hukumu pamoja na “nyumba ya Mungu,” wale wenye kudai kuwa Wakristo. Hivyo Jumuiya ya Wakristo iliyoasi imani ililetwa kwenye jaribio. (Malaki 3:1; 1 Petro 4:17, NW) Hatia ya damu yayo kubwa mno iliyopata wakati wa vita ya ulimwengu ya kwanza, ushiriki wayo katika kunyanyasa mashahidi waaminifu wa Yehova, na itikadi zayo za Kibabuloni havikuisaidia katika wakati wa hukumu yayo; wala hapana sehemu nyingine yoyote ya Babuloni Mkubwa iliyostahili kibali cha Mungu.—Linga Isaya 13:1-9.
-
-
Jiji Kubwa LateketezwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Yeye alikuwa amepata hukumu mbaya ya kimahakama, akingojea kufishwa; kwa hiyo dini bandia haingeweza kushikilia tena watu wa Yehova katika utekwa. (Linga Luka 9:59, 60.) Hao waliachiliwa wakatumikie wakiwa mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu wa Bwana-Mkubwa wakitoa chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa. Wao walikuwa wamepokea hukumu ya ‘Mmefanya vema’ nao walipewa utume wajishughulishe tena na kazi ya Yehova.—Mathayo 24:45-47; 25:21, 23; Matendo 1:8, NW.
-