-
Kudumisha Amani na Usafi wa KutanikoTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
tunalindwa na Yehova kupitia mpango wake wa kitheokrasi chini ya ukichwa wa Kristo. (Zab. 23; Isa. 32:1, 2) Kuwa katika paradiso ya kiroho katika siku hizi zenye taabu kumetufanya tujihisi tukiwa salama.
42 Tunapodumisha amani na usafi wa kutaniko, tunaendelea kuacha nuru yetu ya kweli ya Ufalme iangaze. (Mt. 5:16; Yak. 3:18) Mungu atatubariki, nasi tutashangilia kuona watu wengi zaidi wakimjua Yehova na wakijiunga nasi ili kufanya mapenzi yake.
-
-
Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa KitheokrasiTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 15
Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa Kitheokrasi
NI LAZIMA tujitiishe kwa Mungu, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, ili tuwe sehemu ya tengenezo linalofanya mapenzi ya Yehova. Tunatambua kwamba Mwana wake ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo na pia tunafuata kanuni ya ukichwa katika mambo mengine maishani. Kila mtu anayejitiisha katika mpango huo wa kitheokrasi hufaidika.
2 Wanadamu walijulishwa kwa mara ya kwanza kabisa kuhusu mpango wa kujitiisha chini ya mamlaka katika bustani ya Edeni. Mpango huo unafafanuliwa katika amri za Mungu zilizo kwenye Mwanzo 1:28 na 2:16, 17. Wanyama wangeongozwa na wanadamu, na Adamu na Hawa walipaswa kujitiisha kwa mapenzi na mamlaka ya Mungu. Kutii mamlaka ya Mungu kungeleta amani na utaratibu mzuri. Kanuni ya ukichwa inakaziwa tena katika 1 Wakorintho 11:3. Mtume Paulo aliandika hivi: “Nataka mjue kwamba kichwa cha kila mwanamume ni Kristo; nacho kichwa cha mwanamke ni mwanamume; nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.” Hilo linaonyesha kwamba kila mtu yuko chini ya ukichwa fulani katika mpango huo, isipokuwa Yehova.
3 Watu wengi leo hawaheshimu wala kutii kanuni ya ukichwa. Kwa nini? Tatizo lilianzia Edeni wazazi wa wanadamu walipochagua kimakusudi kutojitiisha chini ya ukichwa wa Mungu mwenye enzi kuu. (Mwa. 3:4, 5)
-