-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Lakini wanaobaki waliuliwa mbali kwa upanga mrefu wa mmoja aketiye juu ya farasi, upanga ambao ulitokeza katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba sehemu zenye mnofu zao.”—Ufunuo 19:19-21, NW.
-
-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
25. (a) Ni nani wale ambao “waliuliwa mbali kwa upanga mrefu wa mmoja aketiye juu ya farasi”? (b) Je! tutazamie kwamba hao waliouliwa mbali watakuwa na ufufuo?
25 Wengine wote ambao hawakuwa sehemu ya serikali moja kwa moja lakini hata hivyo walikuwa sehemu isiyoongoleka ya ulimwengu huu mfisadi wa aina ya binadamu, wao hali kadhalika ‘wanauliwa mbali kwa upanga mrefu wa mmoja aketiye juu ya farasi.’ Yesu atawatamka kuwa wanastahili kifo. Kwa kuwa kwa habari yao ziwa la moto halikutajwa, je! tutaraji kwamba watafufuliwa? Hakuna mahali tunapoambiwa kwamba wenye kufishwa wakati huo na Hakimu wa Yehova wanapaswa kufufuliwa. Kama Yesu mwenyewe alivyotaarifu, wote wale ambao si “kondoo” wanaenda zao “katika moto wa milele uliotayarishwa kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake,” yaani, “katika kukatiliwa mbali kwa milele.” (Mathayo 25:33, 41, 46, NW) Hii huileta kwenye upeo “siku ya hukumu na ya kuharibiwa kwa watu wasiohofu Mungu.”—2 Petro 3:7; Nahumu 1:2, 7-9; Malaki 4:1, NW.
-