-
Acha “Sheria ya Fadhili Zenye Upendo” Ilinde Ulimi WakoMnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
-
-
Fadhili za kawaida, au fadhili za kibinadamu, zinaweza kuonyeshwa hata kwa watu ambao hatuwajui. Mtume Paulo pamoja na watu wengine 275 ambao walivunjikiwa na meli walionyeshwa fadhili kama hizo na wakaaji wa kisiwa cha Malta—watu ambao hawakuwa wamewahi kukutana nao. (Mdo. 27:37–28:2) Kwa upande mwingine, fadhili zenye upendo zinahusisha kushikamana kwa ushikamanifu kati ya watu ambao tayari wamesitawisha uhusiano.a
-
-
Acha “Sheria ya Fadhili Zenye Upendo” Ilinde Ulimi WakoMnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
-
-
9. Ni sababu gani nzuri sana inayowachochea waabudu wa Yehova kuonyesha fadhili zenye upendo katika maisha yao ya kila siku?
9 Mifano mbalimbali katika Maandiko inafunua kwamba Yehova anawaonyesha fadhili zenye upendo, yaani, upendo wake mshikamanifu wale ambao tayari wana msimamo wenye kukubalika mbele zake. Namna gani wale ambao hawana uhusiano kama huo pamoja na Mungu aliye hai? Je, Yehova ni mkali kuwaelekea au hawatendei kwa fadhili? Hapana. “[Mungu] ni mwenye fadhili kuwaelekea wasio na shukrani na waovu,” linasema andiko la Luka 6:35. “Yeye hulichomoza jua lake juu ya watu waovu na wema na hunyesha mvua juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.” (Mt. 5:45) Kabla hatujajifunza kweli na kuanza kutenda kulingana na kweli hiyo, Mungu alikuwa akitutendea kwa fadhili, au kutuonyesha fadhili za kawaida. Hata hivyo, tukiwa waabudu wake tunafaidika na upendo wake mshikamanifu, yaani, fadhili zake zenye upendo ambazo hazibadiliki. (Soma Isaya 54:10.)
-