Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ongeza Shangwe na Heshima ya Siku Yako ya Arusi
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • Jumba la Ufalme—Mahali Panapoheshimiwa

      Inapowezekana, wenzi wengi Wakristo hupendelea arusi yao ifanyiwe katika Jumba la Ufalme. Kwa nini wao hupendelea Jumba la Ufalme? Wenzi fulani walieleza sababu yao: “Tulitambua kwamba ndoa ni mpango mtakatifu wa Yehova. Kufunga ndoa katika Jumba la Ufalme, mahali petu pa ibada, kulikazia akilini mwetu tangu mwanzo kwamba Yehova anapaswa kuwa sehemu ya ndoa yetu. Faida nyingine ya kufanyia arusi katika Jumba la Ufalme badala ya mahali pengine ni kwamba watu wetu wa ukoo wasio waamini ambao walihudhuria waliona jinsi tunavyothamini sana ibada ya Yehova.”

      Wazee wa kutaniko wanaohusika wakikubali Jumba la Ufalme litumiwe kwa ajili ya arusi, wenzi hao wanapaswa kuwajulisha mapema kuhusu matayarisho yatakayofanywa. Njia moja ambayo bibi na bwana-arusi wanaweza kuonyesha kwamba wanawaheshimu wale walioalikwa kwenye arusi ni kuazimia kabisa kufika kwa wakati. Na bila shaka, wanapaswa kuhakikisha kwamba mambo yote yanafanywa kwa njia ya heshima.b (1 Wakorintho 14:40) Hivyo, wataepuka vituko vinavyofanywa katika arusi nyingi za kilimwengu.—1 Yohana 2:15, 16.

      Pia, wale wanaohudhuria arusi wanaweza kuonyesha kwamba wana maoni ya Yehova kuhusu ndoa. Kwa mfano, hawapaswi kutarajia arusi hiyo iwe bora kuliko arusi nyingine za Kikristo, kana kwamba kuna mashindano ya arusi iliyokuwa kubwa. Wakristo wakomavu wanatambua pia kwamba kuwa katika Jumba la Ufalme kwa ajili ya hotuba inayotegemea Biblia ni jambo muhimu na lenye faida zaidi kuliko kuhudhuria karamu ya arusi au tafrija ambayo huenda ikafuata. Ikiwa wakati au hali zinamruhusu Mkristo kuhudhuria tukio moja tu kati ya matukio hayo mawili, bila shaka itafaa kuwa katika Jumba la Ufalme. Mzee anayeitwa William anasema hivi: “Ikiwa wageni wanakosa kwenda katika Jumba la Ufalme bila sababu lakini wanaenda kwenye karamu ya arusi baadaye, hilo linaonyesha kwamba hawathamini utakatifu wa tukio hilo. Hata ikiwa hatukualikwa kwenye karamu, tunaweza kuonyesha kwamba tunawaunga mkono bibi na bwana-arusi na kutoa ushahidi mzuri kwa watu wa ukoo wasio waamini kwa kuhudhuria arusi katika Jumba la Ufalme.”

  • Ongeza Shangwe na Heshima ya Siku Yako ya Arusi
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 15
    • b Ikiwa wenzi wa ndoa wanapanga mtu fulani awapige picha au kurekodi tukio hilo katika Jumba la Ufalme, wanapaswa kuhakikisha mapema kwamba hakuna jambo lolote ambalo litafanya arusi yao isiheshimiwe.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki