-
Upanuzi wa Haraka Wahitajiwa kwa Sababu ya Ongezeko KubwaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
-
-
“Njoni Kwangu, . . . Nami Hakika Nitawaburudisha Ninyi”
Upanuzi wa Haraka Wahitajiwa kwa Sababu ya Ongezeko Kubwa
“NJONI kwangu, . . . nami hakika nitawaburudisha nyinyi,” akasema Yesu Kristo. (Mathayo 11:28) Huo ni mwaliko wenye kusisimua kama nini kutoka kwa Kichwa cha kutaniko la Kikristo! (Waefeso 5:23) Tukichunguza maneno hayo kwa uangalifu, tutathamini sana chanzo muhimu cha burudiko—kushirikiana na ndugu na dada zetu wa kiroho katika mikutano ya Kikristo. Bila shaka, twakubaliana na mtunga-zaburi aliyeimba: “Jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja.”—Zaburi 133:1.
Kwa kweli, tunapata marafiki bora zaidi kwenye mikutano hiyo ambapo hali ya kiroho ni salama na yenye kupendeza. Akiwa na sababu nzuri kijana mmoja Mkristo alisema: “Mimi hushinda shuleni, nami huchoka sana. Lakini mikutano ni kama maji yanayopatikana jangwani, ambapo mimi huburudishwa na kupata nguvu za kukabiliana na siku nyingine shuleni.” Kijana mmoja kutoka Nigeria alisema: “Nimeona kwamba kushirikiana kwa ukaribu na watu wanaompenda Yehova hunisaidia kubaki karibu naye.”
Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova popote pale yalipo hutimiza uhitaji mkubwa katika jamii yakiwa vituo vya ibada ya kweli. Katika sehemu nyingi, angalau mara mbili kwa juma kuna mikutano kwenye Jumba la Ufalme, nao wanafunzi wa Biblia hutiwa moyo kuhudhuria mikutano hiyo upesi iwezekanavyo ili wanufaike na burudiko linalotokana na ushirika huo.—Waebrania 10:24, 25.
-
-
Upanuzi wa Haraka Wahitajiwa kwa Sababu ya Ongezeko KubwaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
-
-
Makutaniko yameona kwamba Jumba la Ufalme linapojengwa, wenyeji hutambua kwamba Mashahidi wa Yehova watadumu mahali hapo. Yaonekana kwamba wengi walikuwa wakisitasita kushirikiana na Mashahidi hadi mahali panapofaa pa ibada palipojengwa. Kutaniko la Nafisi nchini Malawi laripoti: “Sasa tuna Jumba zuri la Ufalme linalotoa ushahidi mzuri. Kwa hiyo, ni rahisi kuanzisha mafunzo ya Biblia.”
Washiriki wa Kutaniko la Krake nchini Benin walivumilia dhihaka kali hapo zamani kwa sababu Jumba lao la Ufalme la zamani lilikuwa la hali ya chini likilinganishwa na makanisa fulani. (Picha ya 4) Sasa kutaniko hilo lina Jumba zuri la Ufalme linalowakilisha ibada ya kweli kwa njia nzuri na ya heshima. (Picha ya 5) Kutaniko hilo lilikuwa na wahubiri wa Ufalme 34 na hudhurio la wastani wa watu 73 kwenye mikutano ya Jumapili. Hata hivyo, watu 651 walihudhuria kuwekwa wakfu kwa Jumba la Ufalme. Wengi waliohudhuria walitoka mjini na walivutiwa kuona jinsi Mashahidi walivyojenga jumba hilo kwa muda mfupi. Ofisi ya tawi nchini Zimbabwe iliandika hivi kuhusu mambo ambayo yametokea kwa sababu ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme: “Mwezi mmoja baada ya Jumba la Ufalme kujengwa, kwa kawaida hudhurio huongezeka maradufu.”—Picha ya 6 na ya 7.
Bila shaka, Majumba mengi mapya ya Ufalme yanawaandalia Wakristo waliojiweka wakfu na watu wanaopendezwa mahali pa kupata burudiko la kiroho. “Tunafurahi sana,” akasema Shahidi mmoja huko Ukrainia baada ya kutaniko moja la kwao kuanza kutumia Jumba jipya la Ufalme. “Tulijionea jinsi Yehova anavyowasaidia watu wake.”
-