-
Kuchapa na Kugawanya Neno Takatifu la Mungu MwenyeweMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Miaka 16 baadaye, katikati ya Vita ya Ulimwengu 2, Sosaiti ilianza kuchapa Biblia yote. Kwa kusudi hilo, mabamba ya King James Version yenye marejezo ya pambizoni yalinunuliwa katika 1942 kutoka kwa Kampuni ya A. J. Holman, ya Philadelphia, Pennsylvania. Tafsiri hiyo ya Biblia yote katika Kiingereza ilitokezwa, si kutoka kwa Vulgate ya Latini, bali kutoka kwa wanachuo walioweza kulinganisha tafsiri za mapema na Kiebrania Kiaramu, na Kigiriki cha awali. Konkodansi iliyotayarishwa na watumishi wa Yehova 150 wenye kushirikiana iliongezwa. Hiyo ilibuniwa kipekee ili kusaidia Mashahidi wa Yehova wapate upesi maandiko yanayofaa wanapokuwa katika huduma ya shambani na hivyo watumie Biblia kwa matokeo ikiwa “upanga wa roho,” ili kuondolea mbali na kufunua uwongo wa kidini. (Efe. 6:17, NW) Ili kufanya Biblia ipatikane kwa watu kila mahali kwa gharama ya chini, ilichapwa kwenye matbaa-mabamba-mviringo ya web—jambo ambalo halikuwa limepata kujaribiwa na wachapaji wengine wa Biblia. Kufikia 1992, jumla ya 1,858,368 ya Biblia hizo zilikuwa zimetokezwa.
-
-
Kuchapa na Kugawanya Neno Takatifu la Mungu MwenyeweMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 606]
Chapa ya Watchtower ya “King James Version,” yenye konkodansi iliyobuniwa kipekee (1942)
-