-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Basi Seleuko wa Pili, mwana wa Laodice, akawa mfalme wa Siria.
-
-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
MFALME WA SIRIA ALIPIZA KISASI
23. Kwa nini mfalme wa kaskazini ‘alirudi mpaka nchi yake mwenyewe’ baada ya kuingia katika ufalme wa mfalme wa kusini?
23 Mfalme wa kaskazini alitendaje? Danieli aliambiwa hivi: “Ataingia katika ufalme wa mfalme wa kusini, lakini atarudi mpaka nchi yake mwenyewe.” (Danieli 11:9) Mfalme wa kaskazini—Mfalme Seleuko wa Pili wa Siria—naye pia alishambulia. Aliingia ndani ya “ufalme” au milki ya mfalme wa kusini wa Misri lakini akashindwa. Jeshi lake likiwa limesalia watu wachache tu, Seleuko wa Pili ‘alirudi mpaka nchi yake mwenyewe,’ na kurudi Antiokia, jiji kuu la Siria wapata mwaka wa 242 K.W.K. Alipokufa, mwana wake Seleuko wa Tatu akatawala baada yake.
-