-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Mwana huyo wa Seleuko wa Pili alikusanya majeshi mengi ili akamshambulie mfalme wa kusini, ambaye wakati huo alikuwa Ptolemy wa Nne.
-
-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
Aliyashinda vibaya majeshi ya Mfalme Ptolemy wa Nne na kutwaa majiji mengi ya Yuda.
-
-
Wafalme Wawili WapambanaSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
MAMBO YAGEUKA
25. Ptolemy wa Nne na Antiochus wa Tatu walipigana wapi, na ni nini ‘lililowekwa mikononi’ mwa mfalme wa kusini wa Misri?
25 Sawa na Danieli, twasikiza kwa hamu malaika wa Yehova atabiripo hivi: “Mfalme wa kusini ataingiliwa na ghadhabu, naye atatoka na kupigana naye, yaani, na mfalme wa kaskazini; naye atapanga jeshi kubwa; na jeshi hilo litawekwa mikononi mwake.” (Danieli 11:11) Akiwa na wanajeshi 75,000, mfalme wa kusini, Ptolemy wa Nne, alielekea kaskazini dhidi ya adui. Mfalme wa Siria wa kaskazini, Antiochus wa Tatu, alikuwa ‘amepanga jeshi kubwa’ la watu 68,000 limkabili. Lakini “jeshi” hilo ‘liliwekwa mikononi’ mwa mfalme wa kusini katika pigano huko Raphia, jiji lililo pwani, karibu na mpaka wa Misri.
26. (a) Ni “jeshi” gani lililochukuliwa na mfalme wa kusini katika pigano huko Raphia, na mkataba wa amani uliofanywa huko ulitia ndani nini? (b) Ni katika njia gani Ptolemy wa Nne ‘hakutumia wadhifa wake wenye nguvu’? (c) Mfalme wa kusini aliyefuata alikuwa nani?
26 Unabii huo waendelea kusema hivi: “Atakapokwisha kuchukua lile jeshi, moyo wake utatukuzwa; naye atawaangusha makumi elfu; lakini hataongezewa nguvu [“hatatumia wadhifa wake wenye nguvu,” NW].” (Danieli 11:12) Ptolemy wa Nne, mfalme wa kusini, ‘alichukua’ askari 10,000 wa miguu na askari-wapanda-farasi 300 wa Siria akawaua na kutwaa wafungwa 4,000. Kisha wafalme hao wakafanya mkataba ambamo Antiochus wa Tatu aliachiwa Seleucia, bandari yake ya Siria lakini akapoteza Foinike na Coele-Siria. Kwa sababu ya ushindi huo, moyo wa mfalme wa kusini wa Misri ‘ulitukuzwa,’ hasa dhidi ya Yehova. Ptolemy wa Nne aliendelea kutawala Yuda. Lakini, ‘hakutumia wadhifa wake wenye nguvu’ baada ya ushindi wake dhidi ya mfalme wa kaskazini wa Siria. Badala yake, Ptolemy wa Nne alianza maisha ya ufasiki, na mwana wake mwenye umri wa miaka mitano, Ptolemy wa Tano, akawa mfalme wa kusini aliyefuata miaka kadhaa kabla ya kifo cha Antiochus wa Tatu.
-