Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mapema katika 1944, N. H. Knorr, F. W. Franz, W. E. Van Amburgh, na M. G. Henschel walitumia siku kumi katika Kuba kuimarisha ndugu kiroho humo. Katika pindi hiyo mkusanyiko ulifanywa katika Havana, na mipango ilitolewa kwa ajili ya kuratibu vizuri zaidi kazi ya kuhubiri.

  • Sehemu ya 3—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Katika 1945 na 1946, N. H. Knorr na F. W. Franz walifanya safari zilizowawezesha kusema na kufanya kazi pamoja na Mashahidi katika nchi 24 katika eneo hilo la kuanzia Mexico hadi ncha ya kusini mwa Amerika Kusini pamoja na Karibea. Walitumia binafsi miezi mitano katika sehemu hiyo ya ulimwengu, wakitoa msaada na mwelekezo wa upendo. Katika baadhi ya sehemu hizo walikutana na watu wachache tu wenye kupendezwa. Ili kuwe na mipango ya ukawaida kwa ajili ya mikutano na utumishi wa shambani, walisaidia kibinafsi katika kupanga kitengenezo makutaniko ya kwanza katika Lima, Peru, na Caracas, Venezuela. Mahali popote ambapo tayari mikutano ya kutaniko ilikuwa ikifanywa, waliihudhuria, na pindi kwa pindi, walitoa shauri juu ya jinsi ya kufanya maendeleo katika thamani yayo yenye kutumika kuhusiana na kazi ya kueneza evanjeli.

      Ilipowezekana, mipango ilifanywa ili hotuba za watu wote za Biblia zitolewe wakati wa ziara hizo. Hotuba hizo zilitangazwa sana kwa kutumia mabango yaliyovaliwa na Mashahidi na kwa kugawanya barabarani vikaratasi vya ukaribishaji. Kama tokeo, wale Mashahidi 394 katika Brazili walifurahia kuwa na watu 765 kwenye mkusanyiko wao katika São Paulo. Katika Chile, ambako kulikuwa na wapiga-mbiu wa Ufalme 83, watu 340 walikuja kusikia hotuba iliyokuwa imetangazwa kipekee. Katika Kosta Rika wale Mashahidi wenyeji 253 walifurahia kuwa na jumla ya watu 849 kwenye mikusanyiko yao miwili. Hizo zilikuwa pindi za ushirika wenye uchangamfu miongoni mwa akina ndugu.

      Hata hivyo, lengo halikuwa tu kuwa na mikusanyiko yenye kukumbukwa. Wakati wa safari hizo wawakilishi kutoka makao makuu waliweka mkazo wa pekee juu ya umaana wa kufanya ziara za kuwarudia watu wenye kupendezwa na kuongoza mafunzo ya Biblia nyumbani pamoja nao. Ikiwa watu wangepata kuwa wanafunzi halisi, walihitaji maagizo ya ukawaida kutoka kwa Neno la Mungu. Kama tokeo, idadi ya mafunzo ya Biblia nyumbani yaliongezeka kasi katika sehemu hiyo ya ulimwengu.

      Wakati Ndugu Knorr na Ndugu Franz walipokuwa wakifanya safari hizo za utumishi, wamishonari zaidi waliozoezwa Gileadi walikuwa wakiwasili katika migawo yao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki