Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wanadamu Wahitaji Ujuzi Juu ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 15
    • 16 Waandikaji katika nchi mbalimbali walitayarisha habari ambayo ilikamilishwa kwa uangalifu kwa ajili ya kitabu Ujuzi. Kwa hiyo kitabu hiki chatazamiwa kuvutia watu wa mataifa yote. Lakini je, itakuwa muda mrefu kabla ya kichapo hiki kutolewa katika lugha za watu kotekote ulimwenguni? La, kwa sababu kitabu cha kurasa 192 chaweza kutafsiriwa upesi zaidi kuliko vitabu vikubwa zaidi. Kufikia Oktoba 1995, Halmashauri ya Uandikaji ya Baraza Linaloongoza ilikuwa imetoa kibali cha utafsiri wa kitabu hiki kutoka Kiingereza hadi lugha zaidi ya 130.

      17. Ni mambo gani yatazamiwayo kufanya iwe rahisi kukitumia kitabu Ujuzi?

      17 Mambo dhahiri katika kila sura ya kitabu Ujuzi yatazamiwa kuwezesha wanafunzi wafanye maendeleo ya kiroho ya haraka zaidi. Kitabu hiki hutoa kweli za Kimaandiko kwa njia chanya. Hakikazii mafundisho bandia. Uwazi wa maneno na ukuzi wa mambo kwa njia ya akili watazamiwa kufanya iwe rahisi kukitumia kitabu hiki ili kuongoza mafunzo ya Biblia na kusaidia watu waelewe ujuzi juu ya Mungu. Zaidi ya maandiko yaliyonukuliwa, kuna maandiko ya Biblia yaliyotajwa ambayo mwanafunzi aweza kuyachunguza katika kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo. Hayo yaweza kusomwa wakati wa funzo kadiri wakati uruhusuvyo, ingawa lisingekuwa jambo la hekima kutia ndani habari ya ziada ambayo ingeweza kuficha mambo makuu. Badala ya hivyo, wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia wapaswa kujaribu kutambua na kupitisha kwa mwanafunzi yale ambayo kitabu kinathibitisha katika kila sura. Hilo lamaanisha kwamba ni lazima mwalimu ajifunze kwa bidii sana, ili mawazo makuu yawe wazi sana akilini mwake.

  • Wanadamu Wahitaji Ujuzi Juu ya Mungu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Januari 15
    • 19. Kabla ya kuongoza mafunzo ya Biblia katika kitabu Ujuzi, kwa nini lingekuwa jambo lenye kusaidia kupitia kurasa 175 hadi 218 katika Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu?

      19 Kitabu Ujuzi kiliandikwa kwa kusudi la kumsaidia mtu ajibu maswali yote ambayo wazee hupitia pamoja na wahubiri wasiobatizwa wanaotaka kubatizwa kuwa Mashahidi wa Yehova. Kwa hiyo, kabla ya kubadilisha mafunzo yako ya Biblia ya sasa kwenye kichapo hiki kipya, inapendekezwa kwamba utumie saa chache ukipitia maswali kwenye kurasa 175 hadi 218 za kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu.a Hilo litakusaidia ukazie majibu kwa maswali hayo wakati wa mafunzo ya Biblia katika kitabu Ujuzi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki