-
Uzuri wa Ziwa Kubwa Zaidi Amerika ya KatiMnara wa Mlinzi—2009 | Septemba 1
-
-
Uzuri wa Ziwa Kubwa Zaidi Amerika ya Kati
INGAWA Nikaragua ni nchi ndogo, ina ziwa kubwa zaidi katika Amerika ya Kati—Ziwa Nikaragua. Jambo la kushangaza ni kwamba huenda Ziwa Nikaragua likawa ndilo ziwa pekee la maji baridi lenye samaki wanaopatikana baharini kama vile papa, chuchunge, na tarpon. Wanasayansi wanaamini kwamba wakati mmoja ziwa hilo lilikuwa ghuba iliyoungana na Bahari ya Pasifiki lakini mlipuko wa volkano ukalitenganisha na bahari. Maji yalipoacha kuwa ya chumvi, samaki walijipatanisha na mazingira yao mapya.
Ziwa hilo lenye urefu wa kilomita 160 na upana wa kilomita 70 hivi, liko mita 30 hivi juu ya usawa wa bahari. Kuna zaidi ya visiwa 400 kwenye Ziwa Nikaragua na visiwa 300 hivi viko kwenye Rasi ya Asese, karibu na mji wa Granada ulioko upande wa kaskazini wa ziwa hilo. Vinaitwa Visiwa Vidogo vya Granada.
Kisiwa kikubwa kwenye ziwa hilo ni Kisiwa cha Ometepe kilichoko katikati. Kisiwa hicho cha Ometepe kilicho na urefu wa kilomita 25 na upana wa kilomita 13, kimefanyizwa kwa milima miwili ya volkano iliyounganishwa kwa shingo ya nchi. Mlima mrefu zaidi wa volkano wenye kilele kilicho na umbo la pia unaitwa Concepción, una kimo cha mita 1,610 juu ya usawa wa ziwa hilo. Huo ni mlima wa volkano hai na unaonekana wazi kabisa upande wa kaskazini wa kisiwa hicho. Mlima ule mwingine unaitwa Madera, nao una kimo cha mita 1,394 na ni volkano isiyotenda. Ukiwa umefunikwa kwa mimea, Mlima Madera una wangwa wenye ukungu ndani ya bonde la mlima huo.
Ziwa Nikaragua ni moja kati ya sehemu ambazo watalii hupenda kutembelea katika eneo hilo. Wao huenda kuona uzuri wa asili wa kitropiki na maeneo ya kiakiolojia ya ustaarabu wa kale. Lakini kuna kitu kingine kuhusu uzuri wa Ziwa Nikaragua ambacho watu wanapaswa kujifunza.
Kijiji Kinachoelea Juu ya Maji
Visiwa Vidogo vya Granada vina mimea mingi ya tropiki na wanyama wengi wa mwituni. Maua maridadi kabisa hukua katika misitu ya visiwa hivi vya volkano. Kwenye fuo za ziwa hilo, utawaona ndege maridadi wa majini kama vile korongo, yangeyange-mkuu, furukombe, mbizi, na mnandi. Kandokando ya misitu hiyo kuna viota vilivyojengwa na ndege wakubwa wanaoitwa Montezuma oropendolas vikining’inia kwenye miti mikubwa vikipeperushwa huku na huku kwa sababu ya upepo unaotoka kwenye ziwa.
Watu wanaishi katika baadhi ya visiwa hivyo vidogo. Kwenye visiwa hivyo utapata nyumba za wavuvi wa eneo hilo na nyumba za matajiri za kuishi wakati wa likizo. Pia, kuna shule na makaburi kwenye visiwa hivyo na vilevile mikahawa na baa. Visiwa hivyo vinafanana na kijiji kinachoelea juu ya maji.
Kila asubuhi mashua yenye rangi ya bluu na nyeupe husafiri kutoka kisiwa kimoja hadi kingine kuwabeba wanafunzi wa shule. Duka linaloelea husafiri kutoka kisiwa kimoja hadi kingine likiwa na matunda na mboga za kuuza. Shughuli za kila siku hutia ndani wanaume kutayarisha nyavu zao na wanawake kufua nguo ziwani.
-
-
Uzuri wa Ziwa Kubwa Zaidi Amerika ya KatiMnara wa Mlinzi—2009 | Septemba 1
-
-
Kisiwa cha Ometepe
Kilomita 50 hivi kuelekea kusini ya Granada, kuna kisiwa cha Ometepe. Tangu zamani watu wamefurahia kuishi kwenye kisiwa hicho kwa sababu ya mazingira yake mazuri na udongo wenye rutuba. Kwa kweli, ukulima nchini Nikaragua ulianza katika kisiwa hicho. Leo, kuna watu 42,000 hivi kwenye kisiwa cha Ometepe ambao huvua samaki na kulima mahindi, ndizi, kahawa, na mazao mengine. Pia, kuna wanyama wengi wa mwitu wenye kupendeza. Kuna kasuku wengi wenye kupiga kelele, magpie-jay wakubwa wakipigapiga mabawa yao yenye manyoya ya bluu na meupe, na tumbili wenye nyuso nyeupe wanaoitwa capuchin wanaopendwa na wengi.
-
-
Uzuri wa Ziwa Kubwa Zaidi Amerika ya KatiMnara wa Mlinzi—2009 | Septemba 1
-
-
Je, Hazina Hizo Zitahifadhiwa?
Ziwa Nikaragua lilionekana kana kwamba haliwezi kuchafuliwa labda kwa sababu ya ukubwa wake. Lakini leo ziwa hilo linahitaji kulindwa. Maji yake yanachafuliwa na uchafu kutoka kwenye mashamba na viwanda na kutoka katika maeneo yaliyokatwa miti.
-