Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Maombolezo
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 1
    • “USIFICHE SIKIO LAKO KWA OMBI LANGU LA KITULIZO”

      (Maombolezo 3:1–5:22)

      Katika Maombolezo sura ya 3, taifa la Israeli linaitwa “mwanamume.” Ingawa amepatwa na taabu, mwanamume huyo anaimba hivi: “Yehova ni mwema kwa yule anayemtumaini, kwa nafsi inayoendelea kumtafuta.” Anamwomba Mungu wa kweli hivi: “Uisikilize sauti yangu. Usifiche sikio lako kwa ombi langu la kitulizo, kwa kilio changu cha kuomba msaada.” Anasema hivi akimwomba Yehova atazame shutuma za adui: “Utawalipa tendo fulani, kulingana na kazi ya mikono yao, Ee Yehova.”—Maombolezo 3:1, 25, 56, 64.

      Yeremia anamwaga hisia zake na kuomboleza hivi kuhusu matokeo mabaya ya kuzingirwa kwa Yerusalemu kwa miezi 18: “Adhabu kwa kosa la binti ya watu wangu pia inakuwa kubwa kuliko adhabu kwa kosa la dhambi ya Sodoma, lililoangamizwa kama kwa dakika moja, na ambalo hakuna mikono iliyojitokeza kulisaidia.” Yeremia anaendelea kusema: “Wale waliouawa kwa upanga wamekuwa bora kuliko wale waliouawa kwa njaa, kwa sababu hao hudhoofika, wakichomwa kwa sababu ya ukosefu wa mazao ya shambani.”—Maombolezo 4:6, 9.

      Katika shairi la tano, wakaaji wa jiji la Yerusalemu ndio wanaozungumza. Wanasema: “Ee Yehova, ukumbuke yale yaliyotupata. Utazame, uone shutuma zetu.” Wanaomba hivi wanaposimulia jinsi walivyotaabika: “Ee Yehova, utaketi mpaka wakati usio na kipimo. Kiti chako cha ufalme ni cha kizazi baada ya kizazi. Uturudishe kwako, Ee Yehova, nasi tutarudi bila kukawia. Utuletee siku zilizo mpya kama katika zamani za kale.”—Maombolezo 5:1, 19, 21.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Maombolezo
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 1
    • Mfanye Yehova Awe Uhakika Wako

      Kitabu cha Biblia cha Maombolezo kinafunua jinsi Yehova alivyoliona jiji la Yerusalemu na nchi ya Yuda baada ya Wababiloni kuliteketeza jiji hilo na kufanya nchi hiyo kuwa ukiwa. Maneno ya kukiri dhambi yaliyo katika kitabu hicho yanaonyesha wazi kwamba kwa maoni ya Yehova, msiba huo ulitukia kwa sababu ya makosa ya watu. Nyimbo za kitabu hiki ambazo ziliongozwa na roho zina maneno yanayoonyesha tumaini katika Yehova na tamaa ya kugeukia njia iliyo sawa. Watu wengi walioishi siku za Yeremia hawakuwa na maoni hayo. Hata hivyo, Yeremia na mabaki waliotubu walikuwa na maoni kama hayo.

      Hatua ya Yehova ya kuchanganua hali ya Yerusalemu kama inavyoonyeshwa katika kitabu cha Maombolezo inatufundisha mambo mawili ya maana sana. Kwanza, kuharibiwa kwa Yerusalemu na kufanywa ukiwa kwa Yuda kunakazia umuhimu wa kumtii Yehova na kutuonya tusipuuze mapenzi yake. (1 Wakorintho 10:11) Jambo la pili tunalojifunza linatokana na mfano wa Yeremia. (Waroma 15:4) Hata katika hali iliyoonekana kuwa haina tumaini, nabii huyo ambaye alikuwa na huzuni nyingi sana alimtegemea Yehova ili amwokoe. Ni muhimu kama nini kwamba tumtegemee kabisa Yehova na Neno lake na kumfanya awe uhakika wetu!—Waebrania 4:12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki