Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutetea Imani Yetu
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
    • Kutetea Kisheria Habari Njema

      18. (a) Kwa nini hatuhitaji ruhusa ya serikali za kibinadamu ili kuhubiri? (b) Sisi huchukua hatua gani tunaponyimwa ruhusa ya kuhubiri?

      18 Mamlaka yetu ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu hutoka mbinguni. Yesu aliyetupa utume wa kufanya kazi hii amepewa “mamlaka yote mbinguni na juu ya dunia.” (Mathayo 28:18-20; Wafilipi 2:9-11) Kwa sababu hiyo, hatuhitaji ruhusa ya serikali za kibinadamu ili kuhubiri. Hata hivyo, sisi hutambua kwamba kuwa na uhuru wa kidini huchangia kuenezwa kwa ujumbe wa Ufalme. Katika nchi ambako tuna uhuru wa kuendelea na ibada yetu, sisi tutatumia utaratibu wa kisheria ili kuulinda. Mahali ambapo tumenyimwa uhuru huo, tutajitahidi kuupata kupatana na utaratibu wa kisheria. Hatukusudii kuongoa jamii, bali “kutetea na kuthibitisha kisheria habari njema.”c—Wafilipi 1:7.

      19. (a) Huenda matokeo ya ‘kumlipa Mungu vitu vya Mungu’ yakawa nini? (b) Tumeazimia kufanya nini?

      19 Tukiwa Mashahidi wa Yehova, twamtambua Yehova kuwa ndiye Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu. Sheria yake ni kuu kuliko zote. Sisi hutii serikali za kibinadamu kwa kudhamiria, hivyo ‘tukimlipa Kaisari vitu vya Kaisari.’ Lakini hatutaruhusu kitu chochote kituzuie tusitimize wajibu ulio muhimu zaidi—‘kumlipa Mungu vitu vya Mungu.’ (Mathayo 22:21) Twaelewa kikamili kwamba kufanya hivyo kutatufanya tuwe “vitu vya kuchukiwa” na mataifa, lakini twakubali jambo hilo kuwa sehemu ya gharama ya kuwa wanafunzi. Rekodi ya kisheria ya Mashahidi wa Yehova katika karne ya 20, ni ushuhuda wa azimio letu la kutetea imani yetu. Kwa msaada na utegemezo wa Yehova, tutaendelea “bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema.”—Matendo 5:42.

  • Kulinda Kisheria Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 1
    • Kulinda Kisheria Habari Njema

      KADIRI ambavyo mwanadamu amekuwa akijenga majiji, ndivyo amekuwa akijenga kuta. Hasa siku zilizopita, ngome hizo zilikuwa ulinzi. Walinzi walipigana wakiwa juu ya vizuizi hivyo, ili kuzuia kuta zisivunjwe wala kudhoofishwa na washambulizi. Kuta hizo zilikuwa ulinzi kwa wakazi wa jiji hilo na pia mara nyingi zilikuwa kimbilio la wakazi wa miji iliyozunguka.—2 Samweli 11:20-24; Isaya 25:12.

      Vivyo hivyo, Mashahidi wa Yehova wamejenga ukuta—ukuta wa kisheria—wa kulinda. Ukuta huo haukujengwa ili kuwatenganisha Mashahidi na jamii iliyosalia, kwa maana Mashahidi wa Yehova wajulikana kwa kuwa watu wenye urafiki, wachangamfu. Badala ya hivyo, umetia nguvu dhamana za kisheria za uhuru wa msingi wa watu wote. Wakati huohuo, ukuta huo hulinda haki za kisheria za Mashahidi ili waweze kuabudu kwa uhuru. (Linganisha Mathayo 5:14-16.) Ukuta huu hulinda njia yao ya kuabudu na haki yao ya kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu. Huo ni ukuta gani, nao umejengwaje?

      Kujenga Ukuta wa Kisheria wa Kulinda

      Ingawa Mashahidi wa Yehova wana uhuru wa ibada katika nchi nyingi, katika nchi fulani wameshambuliwa bila msingi wowote. Uhuru wao wa kuabudu kwa kukusanyika pamoja au kwa kuhubiri nyumba hadi nyumba upingwapo, wamefuatia mambo kisheria. Ulimwenguni pote, kumekuwa na maelfu ya kesi za kisheria zinazohusu Mashahidi.a Hawajapata ushindi katika kesi zote. Lakini mahakama za chini zitoapo uamuzi dhidi yao, mara nyingi wamekata rufani kwenye mahakama za juu zaidi. Kumekuwa na matokeo gani?

      Kwa makumi ya miaka ya karne ya 20, ushindi wa kisheria katika nchi nyingi umeweka vigezo vyenye kutegemeka ambavyo Mashahidi wa Yehova wametumia katika kesi zilizofuata. Sawa na matofali au mawe yanayoufanyiza ukuta, maamuzi hayo yenye kutufaa hufanyiza ukuta wa kisheria wa kulinda. Wakiwa juu ya ukuta huo wa vielelezo, Mashahidi wameendelea kupigania uhuru wao wa kidini wa kuabudu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki