-
Je, Kweli Mungu Anawajali Wanawake?Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 1
-
-
1. Walikuwa na uhuru wa kibinafsi. Tofauti na wanawake katika mataifa mengine mengi ya zamani, wanawake Waisraeli walifurahia uhuru mwingi sana. Ingawa mume alipewa daraka la kuwa kichwa cha familia, mke, akiwa na kibali cha mume wake, ‘angefikiria shamba na kulinunua’ na ‘kupanda shamba la mizabibu.’ Ikiwa alikuwa na ujuzi wa kusokota na kufuma, angeweza hata kufanya biashara yake. (Methali 31:11, 16-19) Chini ya Sheria ya Musa, wanawake walionwa kuwa watu wenye haki za kibinafsi.
-
-
Je, Kweli Mungu Anawajali Wanawake?Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 1
-
-
3. Walistahiwa na kuheshimiwa. Zile Amri Kumi zilisema hivi waziwazi: “Mheshimu baba yako na mama yako.” (Kutoka 20:12) Katika methali za Mfalme Solomoni mwenye hekima, tunasoma hivi: “Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako.”—Methali 1:8.
Sheria ilitia ndani maagizo mengi kuhusu jinsi watu ambao hawajaoana walipaswa kutendeana, na hivyo kuwaheshimu wanawake. (Mambo ya Walawi 18:6, 9; Kumbukumbu la Torati 22:25, 26) Mume mzuri alipaswa kufikiria uwezo wa kimwili na kimaumbile wa mke wake.—Mambo ya Walawi 18:19.
-