Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wenye Shukrani kwa Sababu ya Urithi Wenye Nguvu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Machi 1
    • Migawo ya Mishonari

      Darasa la 16 la Gileadi lilifanyizwa na wanafunzi 120 kutoka sehemu zote za ulimwengu, kutia na wengine waliokuwa wameteseka katika kambi za mateso za Nazi. Kwa kuwa darasa letu lilifundishwa Kihispania, tulitarajia kupewa mgawo wa kwenda baadhi ya nchi zenye watu wanaozungumza Kihispania katika Amerika Kusini. Wazia mshangao wetu siku ya kuhitimu tulipopata kujua kwamba Douglas alipewa mgawo wa kwenda Japani na Anne na mimi kwenda Siria. Kwa hiyo sisi wasichana tulilazimika kujifunza Kiarabu, na ndivyo ilivyokuwa hata wakati ambapo mgawo wetu ulibadilishwa kuwa Lebanoni. Tulipokuwa tukingojea viza zetu, George Shakashiri, mpanga-chapa kamili wa Mnara wa Mlinzi la Kiarabu wa Watch Tower Society, alitufundisha Kiarabu mara mbili kwa juma.

      Ilisisimua kama nini kwenda katika nchi ya Biblia tuliyokuwa tumejifunza juu yake darasani! Keith na Joyce Chew, Edna Stackhouse, Olive Turner, Doreen Warburton, na Doris Wood waliandamana nasi kwenda huko. Tulipata kuwa familia ya mishonari yenye furaha kama nini! Shahidi mwenyeji alizuru makao yetu ya mishonari ili kutusaidia zaidi katika lugha. Wakati wa kipindi cha mafundisho yetu ya kila siku, tulijizoeza utoaji mfupi, ambao baada yake tulienda nje na kuutumia katika kazi yetu ya kuhubiri.

      Tulitumia miaka yetu kadhaa ya kwanza tukiwa Tripoli, ambapo kulikuwa na kutaniko tayari. Joyce, Edna, Olive, Doreen, Doris, Anne, na mimi tuliwasaidia wake na binti za Mashahidi wenyeji kushiriki katika mikutano na pia katika huduma ya waziwazi. Kufikia wakati huo, ndugu na dada zetu Wakristo, wakifuata desturi za huko, hawakuketi pamoja mikutanoni, nao dada hao Wakristo walishiriki katika huduma ya kutoka nyumba hadi nyumba mara chache sana. Tulihitaji usaidizi wao wa lugha katika kuhubiri kwetu waziwazi, nasi tuliwatia moyo kushiriki kazi hiyo wao wenyewe.

      Kisha Anne nami tulipewa mgawo wa kusaidia kikundi kidogo cha Mashahidi katika jiji la kale la Sidoni. Muda mfupi baadaye, tuliombwa kurudi kwenye jiji kuu, Beirut. Mbegu za kweli ya Biblia zilikuwa zimepandwa miongoni mwa jumuiya ya watu wenye kuzungumza Kiarmenia huko, kwa hiyo tulijifunza lugha hiyo ili kuwasaidia.

  • Wenye Shukrani kwa Sababu ya Urithi Wenye Nguvu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi—1998 | Machi 1
    • Familia ya mishonari katika Tripoli, Lebanoni, mwaka wa 1951

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki