-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kwa mara nyingine tena, katika 1990, baada ya vita katika Lebanoni kuacha sehemu za Beirut zikionekana kama kwamba zimepigwa na tetemeko la dunia, wazee miongoni mwa Mashahidi wa Yehova walipanga halmashauri ya kushughulikia utoaji wa kitulizo cha dharura ili kutoa msaada uliohitajiwa kwa akina ndugu. Hawakuwajibika kuuliza wenye kujitolea waje; kila siku wengi walitoa msaada wao.
-
-
Kukua Pamoja Katika UpendoMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 309]
“Nyinyi Mwapendana Kwelikweli”
Baada ya kutazama Mashahidi wenye kujitolea katika Lebanoni yenye kusumbuliwa na vita wakirekebisha kao lililoharibiwa sana la mmoja wa dada zao Wakristo, majirani wake walihisi kusukumwa waulize: “Upendo huu hutoka wapi? Nyinyi ni watu wa aina gani?” Na mwanamke Mwislamu, aliyekuwa akitazama wakati kao la Shahidi mmoja lilipokuwa likisafishwa na kurekebishwa, alijulisha hivi: “Nyinyi mwapendana kwelikweli. Yenu ndiyo dini ya kweli.”
-