-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
11. Kwa nini inafaa kwamba sauti inapaazwa kusema “Mungu wako anamiliki!” kuhusiana na matukio ya mwaka wa 537 K.W.K.?
11 Sasa uangalifu wetu unageuzwa kumwelekea tena Sayuni akiwa bado katika ukiwa wake. Mjumbe anakaribia akiwa na habari njema: “Jinsi ilivyo mizuri [“yenye kupendeza,” “NW”] juu ya milima miguu yake aletaye habari njema, yeye aitangazaye amani, aletaye habari njema ya mambo mema, yeye autangazaye wokovu, auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!” (Isaya 52:7)
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
12. Ni nani aliyeongoza katika ‘kuleta habari njema,’ na jinsi gani?
12 Siku za Isaya, hakuna mtu mmoja au kikundi cha watu kilichotambulishwa kuwa ndicho mtu huyo “aletaye habari njema.” Ingawa hivyo, leo mletaji huyo wa habari njema anajulikana. Yesu Kristo ndiye mjumbe mkubwa zaidi wa amani wa Yehova. Alipokuwa duniani, alizihubiri habari njema kwamba watu wangefunguliwa kabisa wasiwe na madhara ya dhambi iliyorithiwa kutoka kwa Adamu, baadhi yake yakiwa ni magonjwa na kifo. (Mathayo 9:35) Yesu aliweka mfano kwa kutia bidii kuzitangaza habari njema hizo za kitu kizuri zaidi, akatumia kila nafasi aliyopata kuwafundisha watu Ufalme wa Mungu. (Mathayo 5:1, 2; Marko 6:34; Luka 19:1-10; Yohana 4:5-26) Nao wanafunzi wake waliufuata mfano wake.
13. (a) Mtume Paulo anaelezaje kwa upana maana ya usemi ‘Jinsi ilivyo yenye kupendeza juu ya milima miguu yake aletaye habari njema’? (b) Kwa nini inaweza kusemwa kwamba miguu ya wajumbe hao ni “yenye kupendeza”?
13 Katika barua yake kwa Waroma, mtume Paulo ananukuu Isaya 52:7 kukazia umuhimu wa kazi ya kuzihubiri habari njema. Anatokeza mfululizo wa maswali yanayoamsha fikira, mojawapo likiwa ni ‘Watu watasikiaje bila mtu fulani kuhubiri?’ Halafu anasema hivi: “Kama vile imeandikwa: ‘Jinsi ilivyo yenye kupendeza miguu ya wale watangazao habari njema ya mambo mema!’” (Waroma 10:14, 15) Hivyo Paulo anapanua matumizi ya Isaya 52:7, akitumia neno “wale” kwa wingi, badala ya neno “yule” kwa umoja, linalopatikana katika maandishi-awali ya Isaya. Wakristo wote ni wajumbe wa habari njema za amani kwa kumwiga Yesu Kristo. Miguu yao ‘inapendeza’ jinsi gani? Isaya anaongea kana kwamba mpiga-mbiu anakaribia Yerusalemu kutoka kwenye milima ya Yuda iliyo karibu. Haiwezekani kuiona miguu ya mjumbe huyo kwa mbali. Hivyo basi, uangalifu hapa unaelekezwa kwenye mjumbe mwenyewe, kwani ile miguu inawakilisha mjumbe mwenyewe. Sawa na vile Yesu na wanafunzi wake walivyokuwa na sura maridadi kwa watu wasikivu karne ya kwanza, Mashahidi wa kisasa ni wenye kupendeza machoni pa watu wanyenyekevu wanaousikiza ujumbe wa habari njema unaookoa uhai.
-
-
‘Imbeni Pamoja kwa Shangwe’!Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Ni tangu mwaka wa 1919. Mwaka huo, kwenye mkusanyiko fulani Cedar Point, Ohio, J. F. Rutherford, msimamizi wa Watch Tower Society wakati huo, aliwachochea wasikilizaji wake kwa hotuba yenye kichwa “Hotuba kwa Wafanyakazi Wenzi.” Hotuba hiyo, ambayo msingi wake ulikuwa Isaya 52:7 na Ufunuo 15:2, iliwatia moyo wahudhuriaji wote waanze kazi ya kuhubiri. Hivyo, ‘miguu yenye kupendeza’ ilianza kuonekana ‘milimani.’ Kwanza Wakristo watiwa-mafuta, na baadaye waandamani wao wa “kondoo wengine,” walijitokeza kwenda kuzihubiri habari njema kwamba Yehova amekuwa Mfalme. (Yohana 10:16)
-