-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Wakati huo, Veijo Kuismin na mke wake, Sirpa, walikuwa wamishonari huko. Veijo anasema: “Ni ndugu wachache tu walioumia wakati wa vita hivyo, nasi tulipanga kuwapa msaada wale ambao hawakuwa na chakula na fueli. Hilo liliimarisha zaidi umoja kutanikoni na hudhurio likaongezeka nchini kote.”
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Wamishonari sita, Ndugu na Dada Hüttinger, Ndugu na Dada Nygren, na Ndugu na Dada Paris wanatumikia huko Maseru.
-
-
Afrika Kusini2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Per-Ola na Birgitta Nygren wametumikia wakiwa wamishonari huko Maseru tangu mwaka wa 1993. Birgitta anasimulia jambo lililoonwa ambalo linaonyesha thamani ya magazeti katika kuwasaidia watu: “Katika mwaka wa 1997, nilianza kujifunza na mwanamke anayeitwa Mapalesa. Alianza kuhudhuria mikutano, lakini nyakati nyingine hakuwa nyumbani kwa ajili ya funzo, na mara nyingi alijificha. Niliacha kujifunza naye lakini nikaendelea kumpelekea magazeti kwa ukawaida. Miaka mingi baadaye, alihudhuria mkutano wetu. Alieleza kwamba siku moja alisoma makala katika Mnara wa Mlinzi kuhusu kuzuia hasira. Aliona hilo kuwa jibu kutoka kwa Yehova kwa kuwa yeye na watu wake wa ukoo waligombana sikuzote. Alianza kujifunza tena, naye hajakosa mikutano tangu wakati huo. Pia, alianza kuhubiri kwa bidii.”
-