-
Ulimwengu Usio na Umaskini UnakaribiaMnara wa Mlinzi—2005 | Mei 15
-
-
Hebu ona kisa cha mtu anayeitwa Tukiso, ambaye anaishi katika nchi ya Lesotho, kusini mwa Afrika. Mwaka wa 1998, majeshi kutoka nchi nyingine yaliingia Lesotho ili kukomesha maasi dhidi ya serikali. Kwa sababu ya vita hivyo, maduka yaliporwa, watu wakapoteza kazi, na kukawa na ukosefu mkubwa wa chakula.
Tukiso aliishi katika eneo la mji mkuu lenye umaskini mkubwa sana. Majirani wake wengi walikuwa wamepora maduka ili wapate riziki. Tukiso aliporudi kwenye chumba chake, alipata kwamba mwanamke aliyekuwa akiishi naye anayeitwa Maseiso, alikuwa amepora vyakula vingi. Tukiso alimwambia hivi: “Peleka vitu hivi nje.” Kisha akamweleza kwamba sheria ya Mungu inakataza wizi. Maseiso alitii. Majirani waliwadhihaki na kuchukua vyakula hivyo vilivyoibwa.
Tukiso alifanya hivyo kwa sababu ya mambo aliyokuwa amefundishwa na Mashahidi wa Yehova kupitia funzo la Biblia. Je, alikufa njaa kwa sababu ya kutii sheria ya Mungu? La. Baadaye, wazee wa kutaniko la Mashahidi wa Yehova aliloshirikiana nalo waliwasiliana naye na kumletea chakula. Mashahidi wa Yehova katika nchi jirani ya Afrika Kusini walikuwa wametuma zaidi ya tani mbili za chakula ili kuwasaidia ndugu na dada zao Wakristo nchini Lesotho. Maseiso alivutiwa na jinsi Tukiso alivyomtii Mungu na msaada wenye upendo kutoka kwa kutaniko hilo. Yeye pia alianza kujifunza Biblia. Baadaye, walifunga ndoa kisheria, nao wakastahili kubatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Wangali wanamtumikia Mungu kwa uaminifu.
-
-
Ulimwengu Usio na Umaskini UnakaribiaMnara wa Mlinzi—2005 | Mei 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 5]
Tukiso na Maseiso wakiwa na mmishonari aliyejifunza Biblia pamoja na Tukiso
[Picha katika ukurasa wa 5]
Maseiso akiwa mlangoni pa nyumba yake pamoja na mmishonari aliyejifunza Biblia pamoja naye
-