-
Sayansi na Kitabu cha MwanzoUhai—Ulitokana na Muumba?
-
-
Kwa mfano, kabla ya “siku” ya kwanza ya uumbaji, mwanga wa jua, ambalo tayari lilikuwako, haukuwa ukifika duniani, labda kwa sababu ya mawingu mazito. (Ayubu 38:9) Katika “siku” ya kwanza, mawingu hayo yalianza kutanzuka na kuuruhusu mwanga upenye angani.a
Katika “siku” ya pili, yaonekana kwamba anga lilizidi kutanzuka na kutokeza mgawanyiko kati ya mawingu mazito yaliyo juu na bahari. Katika “siku” ya nne, anga lilikuwa limetanzuka vya kutosha hivi kwamba jua na mwezi vingeweza kuonekana “katika anga la mbingu.” (Mwanzo 1:14-16) Yaani, kwa mtu aliye duniani, jua na mwezi vilianza kuonekana. Yote hayo yalitukia hatua kwa hatua.
-
-
Sayansi na Kitabu cha MwanzoUhai—Ulitokana na Muumba?
-
-
a Katika masimulizi kuhusu “siku” ya kwanza, neno la Kiebrania linalotafsiriwa mwanga ni ’ohr, linaloweza kurejelea mwanga wowote ule, lakini kuhusu “siku” ya nne, neno lililotumiwa ni ma·’ohrʹ, linalorejelea chanzo cha mwanga..
-