Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hekima ya Yehova Inaonekana Katika Uumbaji
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • “Shikamaneni na Mema”

      17. Kwa nini miguu ya mjusi inaweza kushika kabisa sehemu laini?

      17 Ni kana kwamba mjusi ana uwezo kuliko nguvu za uvutano. (Soma Methali 30:28.) Kwa kweli, wanasayansi wanashangazwa na uwezo wa kiumbe huyo mdogo wa kupanda kuta na hata kutembea kwenye madari laini bila kuanguka. Ni nini kinachomwezesha mjusi kufanya hivyo? Mjusi hana gundi fulani ya pekee au vidude vya kufyonza hewa. Badala yake, kwenye kila kidole cha mguu wake kuna sehemu zilizoinuka ambazo zina maelfu ya vitu kama nywele. Vitu hivyo vina mamia ya nyuzinyuzi ambazo zina ncha zenye umbo la sahani ndogo. Nguvu za molekuli za nyuzi hizo zote zinaweza kutegemeza uzito unaozidi uzito wa mwili wa mjusi, hata anapotembea tumbo juu kwenye kioo! Watafiti wameshangazwa na uwezo huo wa mjusi, nao wanasema kwamba gundi zenye nguvu zinaweza kutengenezwa kwa kuiga miguu ya mjusi.e

      18. Tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba sikuzote ‘tunashikamana na mema’?

      18 Tunaweza kujifunza nini kutokana na mjusi? Biblia inatuhimiza hivi: “Chukieni maovu, shikamaneni na mema.” (Rom. 12:9) Uvutano mbaya uliopo katika ulimwengu wa Shetani unaweza kutufanya tuache kushikamana na kanuni za Mungu. Kwa mfano, kushirikiana na watu wasiofuata sheria za Mungu, iwe ni shuleni au kazini au kupitia burudani inayomchukiza Mungu, kunaweza kudhoofisha azimio letu la kutenda mema. Usikubali kamwe hilo likupate! Neno la Mungu linaonya hivi: “Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe.” (Met. 3:7) Badala yake, fuata shauri la hekima ambalo Musa aliwapa watu wa Mungu zamani za kale: “Unapaswa kumwogopa Yehova Mungu wako. Unapaswa kumtumikia yeye, nawe unapaswa kushikamana naye.” (Kum. 10:20) Tukishikamana na Yehova, tutakuwa tunamwiga Yesu, ambaye Biblia inasema hivi kumhusu: “Uliupenda uadilifu, nawe ukauchukia uasi-sheria.”—Ebr. 1:9.

  • Hekima ya Yehova Inaonekana Katika Uumbaji
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • [Picha katika ukurasa wa 18]

      Kama mjusi anavyojishikilia kabisa kwenye sehemu mbalimbali, ndivyo Wakristo wanavyoshikamana na mema

      [Hisani]

      Stockbyte/Getty Images

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki