Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hekima ya Yehova Inaonekana Katika Uumbaji
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • Kuvumilia Upinzani

      14. Ingawa huenda tusimstaajabie nzige mmoja, tunaweza kusema nini kuhusu kundi la nzige?

      14 Tunaweza pia kujifunza mambo fulani kutokana na nzige. Huenda tusimstaajabie nzige mmoja tu, ambaye kwa kawaida ana urefu wa sentimita tano hivi, lakini kwa hakika kundi la nzige linastaajabisha. (Soma Methali 30:27.) Kwa kuwa nzige wanakula chakula kingi sana, kundi la wadudu hao wasiochoka linaweza kuharibu haraka shamba lililo tayari kuvunwa. Katika Biblia, sauti ya kundi la wadudu wanaovamia, kutia ndani nzige, inalinganishwa na sauti ya magari ya vita na sauti ya miali ya moto ambayo inateketeza majani makavu. (Yoe. 2:3, 5) Watu wanawasha moto ili kujaribu kuzuia kundi la nzige, lakini kwa kawaida moto unashindwa kuwazuia. Kwa nini? Miili ya nzige waliokufa inazima moto huo, kisha nzige wanaobaki wanasonga mbele bila kizuizi chochote. Hata bila mfalme au kiongozi, kundi la nzige linasonga kama jeshi lililojipanga vizuri, na kushinda kizuizi chochote kile.d—Yoe. 2:25.

      15, 16. Ni kwa njia gani wahubiri wa Ufalme leo ni kama kundi la nzige?

      15 Nabii Yoeli alilinganisha utendaji wa watumishi wa Yehova na utendaji wa nzige. Aliandika hivi: “Wanakimbia kama wanaume wenye nguvu. Wanapanda ukuta kama wanaume wa vita. Nao huenda kila mmoja katika njia zake, nao hawabadili mapito yao. Wala hawasukumani. Wanasonga mbele kama mwanamume katika mwendo wake; na baadhi yao wakianguka katikati ya silaha, wale wengine hawageuzi mwendo wao.”—Yoe. 2:7, 8.

      16 Unabii huo unaeleza vizuri sana kuhusu wahubiri wa Ufalme wa Mungu leo! Hakuna “ukuta” wa upinzani ambao umeweza kusimamisha kazi yao ya kuhubiri. Badala yake, wanamwiga Yesu, ambaye aliendelea kufanya mapenzi ya Mungu hata ingawa wengi walimdharau. (Isa. 53:3) Ni kweli kwamba Wakristo fulani ‘wameanguka katikati ya silaha’ kwa kuuawa kwa sababu ya imani yao. Hata hivyo, kazi ya kuhubiri imeendelea, na idadi ya wahubiri wa Ufalme inaendelea kuongezeka. Kwa kweli, mara nyingi mateso yamesaidia habari njema iwafikie watu ambao hawangesikia kamwe ujumbe wa Ufalme. (Mdo. 8:1, 4) Katika huduma yako, je, unaonyesha uvumilivu kama wa nzige hata unapopata watu wasiopendezwa au wapinzani?—Ebr. 10:39.

  • Hekima ya Yehova Inaonekana Katika Uumbaji
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • [Picha katika ukurasa wa 18]

      Wahudumu Wakristo wanaonyesha uvumilivu kama nzige

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki