Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Washa Upya Upendo wa Kwanza!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 11. (a) Ni kikundi gani cha Kikristo kwenye mandhari ya ulimwengu katika 1918 kilichozoea maneno ya Yesu kwa Waefeso? (b) Jamii ya Yohana ilifanya nini tokea 1919 na kuendelea?

      11 Hata hivyo, ile jamii ya Yohana, iliibuka katika zile siku zenye msukosuko za vita ya kwanza ya ulimwengu ikiwa na upendo kwa ajili ya Yehova na kwa ajili ya ukweli ambao uliwasukuma kumtumikia kwa bidii yenye kuwaka mwali. Wao waliwapinga wale waliojaribu kuingiza faraka kupitia tendo lililokaribia sana kumfanya Charles T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, awe sanamu ya kuabudiwa, kufuatia kifo chake katika 1916. Wakiwa wametiwa nidhamu kwa minyanyaso na misiba, kikundi hiki cha Kikristo kwa wazi kilipokea hukumu ya kupongezwa “umefanya vema” kutoka kwa Bwana-Mkubwa wao pamoja na mwaliko wa kuingia katika shangwe yake. (Mathayo 25:21, 23, NW) Wao walitambua katika mwendo wa matukio ya ulimwengu na katika mambo waliyojionea wenyewe, utimizo wa ile ishara ambayo Yesu alikuwa ametoa ya kutia alama kuwapo kwake kusikoonekana katika uwezo wa Ufalme. Kutoka 1919 na kuendelea, wao walisonga mbele washiriki utimizo zaidi wa unabii mkubwa wa Yesu: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 6:9, 10; 24:3-14, NW) Ikiwa upendo wao kwa Yehova ulikuwa umepungukiwa katika njia fulani, ulipepewa tokea wakati huo na kuendelea ukawa mwali wa moto.

      12. (a) Kwenye mkusanyiko wa kihistoria katika 1922, ni mwito gani uliotokezwa? (b) Ni jina gani walilokubali Wakristo wa kweli katika 1931, na walitubia nini?

      12 Kwenye mkusanyiko wa kihistoria, uliohudhuriwa na 18,000 wa hawa Wakristo, kwenye Sida Pointi, Ohaiyo, U.S.A., Septemba 5-13, 1922, mwito ulitokezwa: “Rudini shambani, Enyi wana wa Mungu aliye juu zaidi sana! . . . Lazima ulimwengu ujue kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. . . . Kwa hiyo vumisheni habari, vumisheni habari, vumisheni habari, ya Mfalme na ufalme wake.” Jina la Yehova lenye thamani kubwa lilikuwa linafanywa kuwa mashuhuri zaidi na zaidi. Katika 1931 Wakristo hawa, wakikusanyika katika mkusanyiko huko Kolumbasi, Ohaiyo, U.S.A., walishangilia kulikubali na kuchukua lile jina alilolionyesha Mungu katika unabii wa Isaya—Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10, 12, NW) Kwa toleo lalo la Machi 1, 1939, jina la jarida kuu la tengenezo hilo lilibadilishwa kuwa Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova, hivyo kumpa heshima ya kwanza Muumba wetu na serikali yake ya kifalme. Mashahidi wa Yehova, wakiwa na upendo kwake uliofanywa upya, wametubia kushindwa kokote ambako huenda wakawa walikuwa nako wakati uliopita katika kuheshimu na kukuza jina lake tukufu na Ufalme wake.—Zaburi 106:6, 47, 48.

  • Washa Upya Upendo wa Kwanza!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • [Sanduku katika ukurasa wa 36]

      Sifa Yenye Upendo kwa Yehova na Mwana Wake

      Katika kitabu cha nyimbo kilichotokezwa na watu wa Yehova katika 1905, mlikuwamo nyimbo mara mbili zilizomsifu Yesu kuliko nyimbo zilizomsifu Yehova Mungu. Katika kitabu chao cha nyimbo cha 1928, hesabu za nyimbo zilizomhimidi Yesu zilikuwa karibu sawa na zile zilizomhimidi Yehova. Lakini katika kile kitabu cha nyimbo cha karibuni zaidi cha 1984, Yehova anaheshimiwa kwa nyimbo nyingi mara nne ya zile zinazomheshimu Yesu. Hili linapatana na maneno ya Yesu mwenyewe: “Baba ni mkuu kuliko mimi.” (Yohana 14:28) Upendo kwa ajili ya Yehova lazima utokezwe mbele zaidi, ukiambatana na upendo wenye kina kirefu kwa ajili ya Yesu na uthamini wa dhabihu yake yenye thamani kubwa na ofisi yake akiwa Kuhani Mkuu na Mfalme wa Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki