-
Udugu Wenye Umoja Usioweza KuvunjwaAmkeni!—2001 | Oktoba 22
-
-
Mipango ya Ujenzi wa Nyumba
Baada ya kuchanganua uharibifu huo, mapendekezo yalifanywa kwa ofisi ya tawi ili kujenga nyumba zilizohitajiwa. Nyumba za muda zilijengwa kwa wale waliopoteza makao yao. Marekebisho yalifanywa pia kwa nyumba ambazo hazikuharibika sana. Wengi walivutiwa na bidii na ustadi wa wafanyakazi wa ujenzi kwani hata majirani walikuja kuwatazama wakifanya kazi.
Mwanamke mmoja akifikiri kwamba wafanyakazi hao walikuwa wale waliotarajiwa kutoka mjini ili kuwasaidia, alilalamika kwamba hakuna aliyemsaidia katika kazi yake ya kufagia vifusi. “La, mama, hawa hawatoki mjini. Ni watu wa Ufalme!” wakaeleza watoto majirani. Moisés Antonio Díaz ambaye si Shahidi pia alisema: “Ni jambo zuri kuona jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyowasaidia walio na uhitaji. Tengenezo hili lina umoja sana, na tunamshukuru Mungu kwamba wana nia ya kutusaidia sisi tulio maskini. Nimefanya kazi pamoja nao na ninanuia kuendelea kufanya hivyo.”
Dada mmoja Mkristo aliyejengewa nyumba alisema hivi kwa machozi: “Mimi na mume wangu tumekosa maneno yafaayo ya kueleza shukrani zetu—kwanza kwa Yehova kisha kwa hawa akina ndugu ambao ijapokuwa hawakutujua walifika bila kukawia ili kutusaidia.”
Kufikia katikati ya mwezi wa Aprili, Mashahidi walikuwa wamewajengea wahasiriwa wa tetemeko la ardhi nyumba 567 na kuandalia karibu familia 100 vifaa vya kurekebisha nyumba zao zilizokuwa zimeharibiwa. Mara tu familia zenye uhitaji zilipopata makao salama, Mashahidi walielekeza uangalifu kwa yale Majumba ya Ufalme 92 yaliyohitaji kurekebishwa au kujengwa upya.
-
-
Udugu Wenye Umoja Usioweza KuvunjwaAmkeni!—2001 | Oktoba 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 26]
Mashahidi walijenga upya Majumba ya Ufalme bila kukawia na kujenga zaidi ya nyumba 500
[Picha katika ukurasa wa 26]
Mama mmoja mwenye shukrani asiye na mume atazama na bintiye nyumba yao iliyoharibiwa ikijengwa upya
-