Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Akawasikitikia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Picha katika ukurasa wa 159

      Onyesha huruma unapohubiri

      17, 18. (a) Ni nini kinachotuchochea tushiriki huduma? (b) Tunaweza kufanya nini ili kukuza sifa ya kuwahurumia wengine?

      17 Tukiwa wafuasi wa Yesu, ni nini kinachotuchochea tushiriki huduma? Kama tulivyoona katika Sura ya 9 ya kitabu hiki, tuna mgawo au kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:19, 20; 1 Wakorintho 9:16) Lakini hatupaswi kushiriki kazi hiyo ili tutimize wajibu tu. Kumpenda Yehova kunatuchochea kuhubiri habari njema ya Ufalme wake. Pia, tunahubiri kwa sababu tunawahurumia wale walio na imani tofauti na yetu. (Marko 12:28-31) Basi, tunaweza kufanya nini ili kukuza sifa ya kuwahurumia wengine?

      18 Tunahitaji kuwaona watu kama Yesu alivyowaona, kwamba “wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.” Hebu wazia umempata mwana-kondoo aliyepotea. Kwa kuwa hana mchungaji wa kumwongoza malishoni na kwenye maji, kiumbe huyo mwenye kusikitisha ana njaa na kiu. Je, hungemhurumia sana mwana-kondoo huyo? Je, hungejitahidi juu chini kumpa chakula na maji? Mwana-kondoo huyo ni kama watu wengi ambao bado hawaijui habari njema. Kwa kuwa wamepuuzwa na wachungaji bandia wa dini, wana njaa na kiu ya kiroho, nao hawana tumaini la kweli la wakati ujao. Tuna kile wanachohitaji, yaani, chakula cha kiroho chenye afya na maji ya kweli yenye kuburudisha yaliyo katika Neno la Mungu. (Isaya 55:1, 2) Tunapofikiria mahitaji ya kiroho ya watu walio karibu nasi, tunawahurumia sana. Tukiwahurumia watu sana kama alivyofanya Yesu, tutajitahidi juu chini kuwaeleza tumaini la Ufalme.

      19. Tunaweza kufanya nini kumchochea mwanafunzi wa Biblia anayestahili kuhubiri hadharani?

      19 Tunaweza kuwasaidiaje wengine wafuate mfano wa Yesu? Tuseme tunataka kumtia moyo mwanafunzi wa Biblia ambaye anastahili kuanza kuhubiri hadharani. Au labda tunataka kumsaidia mhubiri asiyetenda aanze tena kushiriki huduma kikamili. Tunaweza kuwasaidia watu kama hao jinsi gani? Tunapaswa kuchochea mioyo yao. Kumbuka kwamba kwanza Yesu ‘aliwasikitikia’ watu, kisha akawafundisha. (Marko 6:34) Kwa hiyo, ikiwa tunaweza kuwasaidia kusitawisha sifa ya huruma, haikosi mioyo yao itawachochea kumwiga Yesu na kuwahubiria wengine habari njema. Tunaweza kuwauliza: “Ni kwa njia gani kuukubali ujumbe wa Ufalme kumefanya maisha yako yawe bora? Namna gani watu ambao bado hawajaupata ujumbe huo—je, si kweli kwamba wao pia wanahitaji habari njema? Unaweza kuwasaidia jinsi gani?” Bila shaka, kumpenda Mungu na kutaka kumtumikia ndiyo mambo yanayotuchochea zaidi kuhubiri.

      20. (a) Kuwa mfuasi wa Yesu kunatia ndani nini? (b) Tutazungumzia nini katika sura inayofuata?

      20 Kuwa mfuasi wa Yesu kunatia ndani mengi zaidi ya kusema tu maneno aliyosema na kuiga matendo yake. Tunahitaji kuwa na ‘mtazamo wa akili’ aliokuwa nao. (Wafilipi 2:5) Hivyo, tunashukuru kama nini kwamba Biblia inatufunulia maoni na hisia zilizomchochea Yesu kusema na kutenda! Tukiielewa “akili ya Kristo,” tutakuwa wenye kujali na kuwahurumia watu kutoka moyoni, na hivyo kuwatendea wengine kama Yesu alivyowatendea watu kwa ujumla. (1 Wakorintho 2:16) Katika sura inayofuata, tutazungumzia njia mbalimbali ambazo Yesu aliwaonyesha wafuasi wake upendo.

  • “Akawasikitikia”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Unaweza Kumfuata Yesu Jinsi Gani?

      • Yesu alitumiaje mamlaka yake kwa huruma, nasi tunaweza kumwiga jinsi gani?—Mathayo 11:28-30.

      • Kwa nini tunapaswa kufuata mfano wa Yesu kwa kuwaonyesha wengine rehema, au huruma?—Mathayo 9:9-13; 23:23.

      • Ni nini kinachoonyesha kwamba Yesu alielewa hisia za wengine, nasi tunaweza kumwiga jinsi gani?—Luka 7:36-50.

      • Ni kwa njia gani mfano wa Msamaria mwema unaonyesha kwamba huruma ni sifa inayomchochea mtu kutenda, nayo hadithi hiyo inatufundisha nini?—Luka 10:29-37.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki