Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • Kuwatumaini

      15. Kwa nini Yesu aliwatumaini wanafunzi wake ingawa hawakuwa wakamilifu?

      15 Upendo unahusianishwa na tumaini. Upendo “huamini mambo yote.”c (1 Wakorintho 13:7) Upendo wa Yesu ulimsukuma kuwatumaini wanafunzi wake ingawa hawakuwa wakamilifu. Aliwatumaini na kuamini kwamba kwa kweli wanampenda Yehova na wanataka kufanya mapenzi Yake. Hata walipokosea, Yesu hakutilia shaka nia zao. Kwa mfano, pindi moja inaonekana mitume Yakobo na Yohana walimtuma mama yao amwombe Yesu awape mitume hao pendeleo la kuketi kando yake katika Ufalme wake. Hata hivyo, Yesu hakutilia shaka ushikamanifu wao wala kuwanyang’anya pendeleo la kuwa mitume.—Mathayo 20:20-28.

      16, 17. Yesu aliwapa wanafunzi wake kazi gani?

      16 Yesu alionyesha kwamba anawatumaini wanafunzi wake kwa kuwapa kazi mbalimbali. Pindi mbili alipotokeza chakula kingi kimuujiza na kulisha umati wa watu, aliwapa wanafunzi wake kazi ya kugawa chakula hicho. (Mathayo 14:19; 15:36) Aliwapa Petro na Yohana mgawo wa kwenda Yerusalemu na kufanya matayarisho kwa ajili ya Pasaka yake ya mwisho. Walitafuta mwana-kondoo, divai, mkate usio na chachu, mboga chungu za majani, na vitu vingine vya maana vilivyohitajiwa. Huo haukuwa mgawo mdogo, kwa kuwa Sheria ya Musa iliagiza Pasaka iadhimishwe ifaavyo, naye Yesu alihitaji kutii Sheria hiyo. Isitoshe, baadaye usiku huo, Yesu alitumia divai hiyo na mkate huo usio na chachu kuwa mifano muhimu alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake.—Mathayo 26:17-19; Luka 22:8, 13.

      17 Yesu aliwapa wanafunzi wake madaraka mazito hata zaidi. Kama tulivyoona mapema, alikikabidhi kikundi kidogo cha wafuasi wake watiwa-mafuta hapa duniani daraka zito la kutayarisha na kugawa chakula cha kiroho. (Luka 12:42-44) Pia, kumbuka kwamba aliwapa wanafunzi wake kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:18-20) Hata sasa, ingawa anatawala mbinguni na hatuwezi kumwona, Yesu amewapa watu wenye sifa za kiroho, “zawadi katika wanadamu,” daraka la kutunza kutaniko lake lililo duniani.—Waefeso 4:8, 11, 12.

      18-20. (a) Tunaweza kuonyesha jinsi gani kwamba tunawatumaini waamini wenzetu? (b) Ni kwa njia gani tunaweza kuiga mfano wa Yesu wa kuwa tayari kuwapa wengine migawo? (c) Ni nini kitakachozungumziwa katika sura inayofuata?

      18 Tunaweza kumwiga Yesu jinsi gani tunaposhughulika na watu wengine? Kuwatumaini waamini wenzetu kunaonyesha kwamba tunawapenda. Tusisahau kwamba upendo huangalia mambo mazuri bali si mabaya. Wakati ambapo watu wengine wanatuvunja moyo, jambo ambalo mara kwa mara linatokea, upendo utatuzuia tusikate kauli mara moja kwamba nia zao ni mbovu. (Mathayo 7:1, 2) Tukiwa na maoni yanayofaa kuhusu waamini wenzetu, tutawatendea kwa njia zenye kuwajenga badala ya kuwabomoa.—1 Wathesalonike 5:11.

      19 Je, tunaweza kumwiga Yesu kwa kuwa tayari kuwapa wengine mapendeleo? Ndugu walio na madaraka kutanikoni wanapaswa kuwapa wengine migawo inayowafaa na inayotimiza kusudi fulani wakiamini kwamba ndugu hao watafanya yote wanayoweza. Kwa njia hiyo, wazee wenye uzoefu wanaweza kuwazoeza vijana wanaostahili ambao ‘wanajitahidi kufikia’ mapendeleo ya kulisaidia kutaniko. (1 Timotheo 3:1; 2 Timotheo 2:2) Mazoezi hayo ni ya maana. Yehova anapoendelea kuharakisha ukuzi wa Ufalme, wanaume wanaostahili watahitaji kuzoezwa kushughulikia ongezeko hilo.—Isaya 60:22.

  • ‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • c Bila shaka, haimaanishi kwamba upendo ni mpumbavu au unadanganyika upesi. Badala yake, inamaanisha kwamba upendo hauchambui au kuwa na shaka juu ya mambo bila sababu. Upendo huepuka kutilia shaka nia za wengine au kukata kauli kwamba hawana nia nzuri.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki