-
Kufaidika na Fadhili-upendo za YehovaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
-
-
Fadhili-Upendo Ni Tofauti na Upendo na Uaminifu-Mshikamanifu
3. Sifa ya fadhili-upendo inatofautianaje na upendo?
3 Sifa ya fadhili-upendo, au upendo mwaminifu-mshikamanifu, inakaribiana sana na sifa ya upendo na ya uaminifu-mshikamanifu. Hata hivyo, sifa ya fadhili-upendo ni tofauti na sifa hizo nyingine katika njia mbalimbali muhimu.
-
-
Kufaidika na Fadhili-upendo za YehovaMnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
-
-
4. Sifa ya fadhili-upendo inatofautianaje na uaminifu-mshikamanifu?
4 Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “fadhili-upendo” pia lina maana pana zaidi kuliko usemi “uaminifu-mshikamanifu.” Katika lugha fulani, usemi “uaminifu-mshikamanifu” hutumiwa mara nyingi kuonyesha jinsi mfanyakazi anavyopaswa kutenda kuelekea mkubwa wake. Lakini mtafiti mmoja anasema kwamba ‘mara nyingi Biblia hutumia usemi fadhili-upendo kuonyesha uhusiano ulio tofauti na wa mfanyakazi na mkubwa wake: yaani, mkubwa anakuwa mwaminifu-mshikamanifu kwa aliye mnyonge na mwenye uhitaji.’ Hivyo mfalme Daudi angeweza kumwomba Yehova hivi: “Umwangaze mtumishi wako kwa nuru ya uso wako. Uniokoe kwa ajili ya fadhili [“fadhili-upendo,” NW] zako.” (Zaburi 31:16) Yehova, ambaye ndiye mwenye uwezo, anaombwa aonyeshe fadhili-upendo, au upendo mwaminifu-mshikamanifu kwa Daudi mwenye uhitaji. Kwa kuwa wenye uhitaji hawana mamlaka juu ya wenye uwezo, sifa ya fadhili-upendo katika uhusiano kama huo inaonyeshwa kwa nia ya kupenda wala si kwa kulazimishwa.
-