Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kufaidika na Fadhili-upendo za Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
    • Fadhili-Upendo Ni Tofauti na Upendo na Uaminifu-Mshikamanifu

      3. Sifa ya fadhili-upendo inatofautianaje na upendo?

      3 Sifa ya fadhili-upendo, au upendo mwaminifu-mshikamanifu, inakaribiana sana na sifa ya upendo na ya uaminifu-mshikamanifu. Hata hivyo, sifa ya fadhili-upendo ni tofauti na sifa hizo nyingine katika njia mbalimbali muhimu.

  • Kufaidika na Fadhili-upendo za Yehova
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Mei 15
    • 4. Sifa ya fadhili-upendo inatofautianaje na uaminifu-mshikamanifu?

      4 Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “fadhili-upendo” pia lina maana pana zaidi kuliko usemi “uaminifu-mshikamanifu.” Katika lugha fulani, usemi “uaminifu-mshikamanifu” hutumiwa mara nyingi kuonyesha jinsi mfanyakazi anavyopaswa kutenda kuelekea mkubwa wake. Lakini mtafiti mmoja anasema kwamba ‘mara nyingi Biblia hutumia usemi fadhili-upendo kuonyesha uhusiano ulio tofauti na wa mfanyakazi na mkubwa wake: yaani, mkubwa anakuwa mwaminifu-mshikamanifu kwa aliye mnyonge na mwenye uhitaji.’ Hivyo mfalme Daudi angeweza kumwomba Yehova hivi: “Umwangaze mtumishi wako kwa nuru ya uso wako. Uniokoe kwa ajili ya fadhili [“fadhili-upendo,” NW] zako.” (Zaburi 31:16) Yehova, ambaye ndiye mwenye uwezo, anaombwa aonyeshe fadhili-upendo, au upendo mwaminifu-mshikamanifu kwa Daudi mwenye uhitaji. Kwa kuwa wenye uhitaji hawana mamlaka juu ya wenye uwezo, sifa ya fadhili-upendo katika uhusiano kama huo inaonyeshwa kwa nia ya kupenda wala si kwa kulazimishwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki