Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa Moto
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • “Wale wote ambao mimi naonea shauku mimi nakaripia na kunidhamu. Kwa hiyo uwe mwenye bidii na kutubu.” (Ufunuo 3:19, NW) Kama vile nidhamu kutoka kwa Yehova, nidhamu ya Yesu ni ishara ya upendo. (Waebrania 12:4-7) Kundi la Laodikia lapaswa lijifaidi na hangaikio lake lenye shauku na kutumia shauri lake. Inawapasa watubu wakitambua kwamba uvuguvugu wao ni kutenda dhambi. (Waebrania 3:12, 13; Yakobo 4:17) Acha wazee walo waweke nyuma njia za kufuatilia vitu vya kimwili na ‘kuchochea kama moto’ ile karama waliyo nayo kutoka kwa Mungu. Ile dawa ya macho ikiwa inafanya kazi, acha wote waliomo katika kundi hilo wapate burudisho kama lile linalotokana na kinywaji cha maji baridi kutoka chemchemi ya maji.—2 Timotheo 1:6; Mithali 3:5-8; Luka 21:34.

  • Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa Moto
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 17. Utajiri unaweza kuwaje hatari kwetu kiroho?

      17 Lazima sisi tusiruhusu ufuatiaji wa vitu vya kimwili, mali, au ukosefu wa mali utufanye sisi tuwe wenye uvuguvugu. Utajiri unaweza kusaidia kufungulia uwezekano mpya ulio mwingi wa utumishi, lakini pia unaweza kuwa hatari. (Mathayo 19:24) Mtu mwenye mali huenda akahisi kwamba yeye hahitaji kuwa mwenye bidii katika kazi ya kuhubiri kama wengine, mradi yeye anatoa michango mikubwa wakati kwa wakati. Au huenda akahisi kwamba kuwa tajiri kunampa haki ya kupata mapendeleo. Kwa kuongezea, kuna raha na maburudisho ambayo yako wazi kwa mtu tajiri ambayo wengine hawawezi kuyapata. Lakini tafrija hizo huchukua wakati na zaweza kuvuta mtu asiyejihadhari mbali na huduma ya Kikristo, hivyo kumfanya huyo asiye mwangalifu kuwa mwenye uvuguvugu. Sisi na tujiepushe na mitego hiyo yote na tuendelee “kufanya kazi sana na kujipinda wenyewe” kwa moyo wote, tukiutazamia uhai wa milele.—1 Timotheo 4:8-10; 6:9-12, NW.

      “Kutwaa Mlo wa Jioni”

      18. Ni fursa gani ambayo Yesu anaweka mbele ya Wakristo katika Laodikia?

      18 Yesu anaendelea kusema: “Tazama! Mimi ninasimama penye mlango na kubisha. Ikiwa ye-yote asikia sauti yangu na kufungua mlango, mimi nitaingia ndani ya nyumba yake na kutwaa mlo wa jioni pamoja na yeye na yeye pamoja na mimi.” (Ufunuo 3:20, NW) Ikiwa Wakristo hao Walaodikia wanamkaribisha Yesu ndani ya kundi lao, yeye atawasaidia washinde uvuguvugu wao!—Mathayo 18:20.

  • Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa Moto
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 20. (a) Mwanzoni mwa ile siku ya Bwana, ni jambo gani lililotokezwa na uvuguvugu wa Jumuiya ya Wakristo? (b) Hukumu ya Yesu imeathirije Jumuiya ya Wakristo?

      20 Waidha lenye upendo la Yesu kwa Walaodikia lina maana kubwa kwa mabaki ya Wakristo wapakwa-mafuta leo. Wengine wao wanakumbuka kwamba, ile siku ya Bwana ilipokuwa ikianza, wanadini wa Jumuiya ya Wakristo walikuwa wenye uvuguvugu kwa kiwango chenye kusikitisha sana. Badala ya kukaribisha kurudi kwa Bwana yetu katika 1914, viongozi wa kidini wayo walijiingiza sana katika ule mchinjo wa Vita ya Ulimwengu 1, ambayo katika hiyo mataifa 24 kati ya yale 28 yaliyokuwa yakipigana yalidai kuwa ya Kikristo.

  • Nunua Dhahabu Iliyosafishwa kwa Moto
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 21. Kutoka 1919 na kuendelea, Wakristo katika kundi la kweli wameitikiaje maneno ya Yesu kwa Wakristo katika Laodikia?

      21 Hata ndani ya lile kundi la kweli, mmekuwamo watu mmoja mmoja ambao wako kama kinywaji ambacho si chenye moto wenye kuchochea wala chenye baridi yenye kuburudisha. Lakini Yesu angali anapenda kichangamfu kundi lake. Yeye anajifanya mwenyewe apatikane kwa Wakristo wanaoitikia kwa ukaribishaji-wageni, na wengi wamemkaribisha, kana kwamba kwa mlo wa jioni. Kama tokeo, tangu 1919 na kuendelea macho yao yamefunguliwa yaone maana ya unabii wa Biblia. Wao wamefurahia kipindi cha nuru ya elimu kubwa.—Zaburi 97:11; 2 Petro 1:19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki