Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Akiwa na umri wa miaka 18, Magdalena, aligunduliwa kuwa ana ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili (systemic lupus erythematosus). Inaonekana kwamba katika ugonjwa huo, kinga ya mwili hushambulia viungo vya mwili. Magdalena anasema hivi: “Niliogopa sana, kadiri wakati ulivyopita ndivyo hali yangu ilivyozidi kudhoofika na hali ikawa mbaya zaidi kwa sababu ya matatizo ya kutomeng’enya chakula vizuri, vidonda vya mdomoni, na matatizo ya koo.”

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Magdalena anasema hivi: “Ugonjwa nilionao unazidi kuwa mbaya. Mara kwa mara ninajihisi nimechoka sana nisiweze kutoka kitandani. Kwa sababu ya hali isiyotabirika ya ugonjwa wangu, ni vigumu sana kupanga mambo ya baadaye. Jambo linalonivunja moyo sana ni kwamba siwezi tena kufanya mengi katika utumishi wa Yehova kama nilivyokuwa nikifanya zamani.”

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Kwa kumtegemea Mungu kupitia sala, Magdalena anaendelea kukabiliana na ugonjwa wake wenye kudhoofisha. Anasema hivi: “Kumweleza Yehova yaliyo moyoni mwangu hunituliza na kunirudishia shangwe yangu. Kwa kweli, sasa ninaelewa kumtegemea Mungu siku kwa siku kunamaanisha nini.”—2 Kor. 1:3, 4.

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Magdalena anaeleza hivi: “Kutaniko limehakikisha kwamba ninafaidika na mikutano kwa kunirekodia mikutano. Mara kwa mara waamini wenzangu hunipigia simu ili kujua jinsi wanavyoweza kunisaidia. Pia, wao hunitumia kadi zinazotia moyo. Kujua kwamba ndugu na dada wananikumbuka na kujali hali yangu hunisaidia kuendelea kuvumilia.”

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • Magdalena anasema hivi: “Ninajitahidi sana ili nisiyakazie fikira matatizo yangu. Mimi hujitahidi kufurahia siku ambazo ninajihisi vizuri. Ninatiwa moyo sana ninaposoma masimulizi ya maisha ya watu ambao wamebaki wakiwa waaminifu licha ya magonjwa yao ya kudumu.” Izabela anaimarishwa kwa kujua kwamba Yehova anampenda na kumthamini sana. Anasema hivi: “Ninahisi kwamba ninahitajika, na kwamba nina mtu ambaye ninaweza kutumia maisha yangu kwa ajili yake. Pia, nina tumaini zuri ajabu la wakati ujao.”

  • Usiruhusu Ugonjwa Ukufanye Upoteze Shangwe Yako
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Desemba 15
    • “Zaidi ya kutoa ushahidi kwa simu, mimi pia huandika barua na kwa kawaida ninawasiliana na watu wachache wanaopendezwa. Nyakati zote ninapokuwa hospitalini mimi huweka Biblia na machapisho kando ya kitanda changu. Hilo limenisaidia kuanzisha mazungumzo mengi mazuri.”—Magdalena, ambaye amegunduliwa kuwa ana ugonjwa wa mfumo wa kinga ya mwili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki