Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mkusanyiko uliratibiwa katika Pittsburgh, Pennsylvania, Januari 2-5, 1919, wakati ambao Ndugu Rutherford na washirika wake walikuwa gerezani. Lakini huu haukuwa mkusanyiko wa kawaida—uliunganishwa na mkutano wa kila mwaka wa Watch Tower Society, Jumamosi, Januari 4, 1919. Ndugu Rutherford alijua vema umaana wa mkutano huo. Alasiri ya Jumamosi hiyo yeye alimtafuta Ndugu Macmillan na kumpata kwenye uwanja wa tenisi wa gereza. Kulingana na Macmillan, ilitukia hivi:

      “Rutherford alisema, ‘Mac, nataka kuongea nawe.’

      “‘Wataka kuongea nami juu ya nini?’

      “‘Nataka kuongea nawe juu ya yale yanayotukia katika Pittsburgh.’

      “‘Ningependa kumaliza mchezo huu hapa.’

      “‘Je, wewe hupendezwi na yanayotukia? Wewe hujui leo uchaguzi wa maofisa unafanywa? Huenda ukapitwa na kukataliwa nasi tutakaa humu milele.’

      “‘Ndugu Rutherford,’ nikasema, ‘acha nikuambie jambo ambalo labda hujalifikiria. Hii ndiyo mara ya kwanza tangu Sosaiti ilipoandikishwa kuwa shirika ambapo inaweza kuwa wazi ni nani ambaye Yehova Mungu angetaka awe msimamizi.’

      “‘Wamaanisha nini?’

      “‘Namaanisha kwamba Ndugu Russell alikuwa na kura ya uamuzi naye aliweka wale maofisa mbalimbali. Sasa kwa kuwa yaonekana sisi hatuwezi kushiriki, mambo ni tofauti. Lakini, tukitoka kukiwa kungali wakati twende kwenye kusanyiko hilo kwenye mkutano huo wa mambo ya kikazi, tungeingia nasi tungekubaliwa tuchukue mahali pa Ndugu Russell kwa heshima ileile aliyopokea. Basi ingeonekana kuwa ni kazi ya mwanadamu, si ya Mungu.’

      “Rutherford alionekana kuwa mwenye kufikiri tu naye akaenda zake.”

  • Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kesho yake Ndugu Rutherford alibisha kwenye ukuta wa seli ya Macmillan na kusema: “Chomoza mkono wako nje.” Kisha akampa Macmillan barua ya simu iliyosema kwamba Rutherford alikuwa amechaguliwa tena kuwa msimamizi. “Alikuwa mwenye furaha sana,” Macmillan akakumbuka baadaye, “kuona wonyesho huo wa uhakikishio kwamba Yehova alikuwa akiendesha Sosaiti.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki