Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Alexander H. Macmillan, ambaye alikuwa amebatizwa Septemba 1900, alikumbuka baadaye hivi: “Wachache kati yetu tulifikiri kwa uzito sana kwamba tungeenda mbinguni wakati wa juma la kwanza la mwezi huo wa Oktoba.”a Kwa kweli, akikumbuka asubuhi ambayo Russell alitangaza mwisho wa Nyakati za Mataifa, Macmillan alikubali hivi: “Tulisisimka sana sana, nami singeshangaa kama katika nukta hiyo tungeanza tu kupaa, huku tangazo la Russell likiwa ni ishara ya kuanza kupaa kuelekea mbinguni—lakini bila shaka hakukuwa na jambo lolote kama hilo.”

  • Wakati wa Kutahini (1914-1918)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 62]

      “Baadhi Yetu Tulikuwa Tumekuwa Kidogo Wenye Haraka Mno”

      Oktoba 1914 ulipokuwa ukikaribia, baadhi ya Wanafunzi wa Biblia walitarajia kwamba mwishoni mwa Nyakati za Mataifa, wao, wakiwa Wakristo watiwa-mafuta kwa roho, wangepokea thawabu yao ya kimbingu. Kuonyesha hilo ni tukio moja lililotukia katika mkusanyiko mmoja wa Wanafunzi wa Biblia katika Saratoga Springs, New York, Septemba 27-30, 1914. A. H. Macmillan, aliyekuwa amebatizwa miaka 14 mapema, alitoa hotuba Jumatano, Septemba 30. Katika kuitoa aliarifu hivi: “Labda hii ndiyo hotuba ya watu wote ya mwisho ambayo nitapata kutoa kwa sababu tutaenda nyumbani [mbinguni] karibuni.”

      Hata hivyo, siku mbili baadaye (Ijumaa, Oktoba 2), Macmillan alitaniwa kwa uchangamfu katika Brooklyn, ambako wajumbe wa mkusanyiko wangekusanyika tena. Akiwa katika kiti chake kichwani pa meza, C. T. Russell alitangaza hivi: “Tutafanya mabadiliko fulani katika programu ya Jumapili [Oktoba 4]. Wakati wa saa 4:30 asubuhi ya Jumapili Ndugu Macmillan atatutolea hotuba.” Itikio likawaje? Macmillan aliandika baadaye hivi: “Kila mtu aliangua kicheko, wakikumbuka niliyokuwa nimesema Jumatano katika Saratoga Springs—‘hotuba yangu ya mwisho ya watu wote’!”

      “Basi,” Macmillan akaendelea, “wakati huo ikawa lazima nishughulike kupata jambo la kusema. Nilipata Zaburi 74:9, ‘Hatuzioni ishara zetu, wala sasa hakuna nabii, wala kwetu hakuna ajuaye, hata lini.’ Ahaa! Hilo lilikuwa tofauti. Katika hotuba hiyo nilijaribu kuonyesha akina ndugu kwamba labda baadhi yetu tulikuwa tumekuwa kidogo wenye haraka mno katika kufikiri kwamba tungeenda mbinguni mara hiyo, na jambo linalotufaa kufanya ni kuendelea kujishughulisha na utumishi wa Bwana mpaka yeye aamue ni wakati gani yeyote kati ya watumishi wake waliokubaliwa angechukuliwa nyumbani kwenda mbinguni.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki