Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutahini na Kupepeta Kuanzia Ndani
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mmoja wao alikuwa A. H. Macmillan. Baadaye aliandika: “Ingawa mataraja yetu kuhusu kuchukuliwa hadi mbinguni hayakutimizwa katika 1914, mwaka huo ndio uliokuwa mwisho wa Nyakati za Mataifa . . . Hatukusikitika sana hasa kwamba kila kitu hakikutukia kama vile tulivyokuwa tumetazamia, kwa sababu tulikuwa wenye shughuli mno na kazi ya Photo-Drama na matatizo yaliyoletwa na vita.” Yeye aliendelea kuwa mwenye shughuli katika utumishi wa Yehova na alisisimuliwa kuona idadi ya wapiga-mbiu wa Ufalme ikiongezeka kufikia zaidi ya milioni moja wakati wa maisha yake.

      Akitazama nyuma kwenye mambo aliyoona wakati wa miaka 66 katika tengenezo, yeye alisema: “Nimeona majaribu mengi makali yakikumba tengenezo na kutahiniwa kwa imani ya wale waliomo. Kwa msaada wa roho ya Mungu tengenezo liliokoka na likaendelea kusitawi.” Kuhusu marekebisho ya uelewevu kadiri wakati ulivyopita, yeye aliongeza: “Kweli za msingi tulizojifunza kutoka kwa Maandiko zilibaki vilevile. Kwa hiyo nilijifunza kwamba tunapaswa kukubali makosa yetu na kuendelea kutafuta katika Neno la Mungu ili kupata nuru zaidi. Hata iwe ni mabadiliko gani ambayo tungelazimika kufanya wakati mmoja au mwingine katika maoni yetu, hilo halingebadili uandalizi wa fadhili wa fidia na ahadi ya Mungu ya uhai wa milele.”

  • Kutahini na Kupepeta Kuanzia Ndani
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 637]

      A. H. Macmillan

      “Nimeona hekima ya kumngoja Yehova kwa subira ili atueleweshe vizuri zaidi mambo ya Kimaandiko badala ya kukasirika kwa ajili ya wazo jipya. Nyakati nyingine matarajio yetu ya tarehe fulani yalikuwa zaidi ya yale ambayo Maandiko yaliruhusu. Wakati matarajio hayo yalipokosa kutimizwa, hilo halikubadili makusudi ya Mungu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki