-
Tuliazimia Kumtumikia YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Aprili 1
-
-
Ndugu Knorr alinipa mimi na mke wangu mgawo wa umishonari katika Jamhuri ya Malagasi, inayojulikana sasa kama Madagaska. Nilimwandikia Veera na kumuuliza maoni yake kuhusu mgawo huo, naye alijibu mara moja, “Ndiyo.” Niliporudi Finland, tulifanya haraka kujitayarisha kwa ajili ya maisha huko Madagaska.
Shangwe na Kukata Tamaa
Mnamo Januari 1962 tulipanda ndege kwenda Antananarivo, jiji kuu la nchi hiyo. Tulikuwa tumevalia kofia zenye manyoya na makoti mazito, kwa kuwa tuliondoka Finland katika majira ya baridi kali. Tulibadili mavazi yetu upesi kwa sababu ya hali ya joto ya Madagaska. Makao yetu ya kwanza ya wamishonari yalikuwa madogo na yenye chumba kimoja cha kulala. Tayari kulikuwa na wenzi wa ndoa wamishonari katika makao hayo, kwa hiyo mimi na Veera tulilala ukumbini.
Tulianza kujifunza Kifaransa, lugha rasmi ya Madagaska. Haikuwa rahisi kwa kuwa tulizungumza lugha tofauti na ya mwalimu wetu, Dada Carbonneau. Alitufundisha Kifaransa akitumia Kiingereza, lakini Veera hakuwa anajua Kiingereza. Hivyo, nilimtafsiria Veera maagizo ya Dada Carbonneau katika Kifini. Kisha, tukagundua kwamba Veera alielewa mambo magumu ya lugha alipoelezwa kwa Kiswedi. Hivyo, nilimfafanulia sarufi ya Kifaransa kwa kutumia Kiswedi. Baada ya muda mfupi, tulifanya maendeleo mazuri katika Kifaransa, kisha tukaanza kujifunza lugha ya wenyeji ya Kimalagasi.
Mtu wa kwanza niliyejifunza Biblia naye nchini Madagaska alikuwa mwanamume ambaye alizungumza Kimalagasi pekee. Nilisoma mistari katika Biblia yangu ya Kifini kisha tukachunguza mistari hiyo katika Biblia ya Kimalagasi. Ingawa sikuweza kumwelezea mengi kuhusu maandiko hayo, muda si muda mwanamume huyo alianza kuthamini kweli ya Biblia, akafanya maendeleo na kubatizwa.
Katika mwaka wa 1963, Milton Henschel wa makao makuu ya Mashahidi wa Yehova huko Brooklyn, alitembelea Madagaska. Muda mfupi baadaye, ofisi mpya ya tawi ilianzishwa nchini Madagaska, nami nikawekwa kuwa mwangalizi wa tawi, mbali na mgawo wangu wa kuwa mwangalizi wa mzunguko na wa wilaya. Wakati huo wote, Yehova alitubariki sana. Kuanzia mwaka wa 1962 mpaka 1970, idadi ya wahubiri wa Ufalme nchini Madagaska iliongezeka kutoka 85 mpaka 469.
Siku moja mnamo 1970, tuliporudi kutoka mahubiri, tulipata barua mlangoni iliyoamuru wamishonari wote wa Mashahidi wa Yehova wafike kwenye ofisi ya waziri wa mambo ya ndani. Tukiwa huko, ofisa mmoja alituambia kwamba serikali ilikuwa imetoa amri tuondoke nchini mara moja. Nilipouliza kosa linalofanya nifukuzwe, ofisa huyo aliniambia hivi: “Bwana Kuokkanen, hujafanya kosa lolote.”
Nikamwambia: “Tumekuwa hapa kwa miaka minane. Huku ndiko nyumbani. Hatuwezi kuondoka ghafula bila sababu yoyote.” Licha ya jitihada zetu, wamishonari wote walilazimika kuondoka katika kipindi cha juma moja. Ofisi ya tawi ilifungwa, na Shahidi mwenyeji akaanza kusimamia kazi ya kuhubiri. Kabla ya kuwaacha ndugu zetu wapendwa wa Madagaska, tulipata mgawo mpya nchini Uganda.
-
-
Tuliazimia Kumtumikia YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Aprili 1
-
-
Kufikia mwaka wa 1990 upinzani kuelekea kazi ya kuhubiri huko Madagaska ulikuwa umepungua, nasi tulishangaa wakati makao makuu ya Brooklyn yalipotuomba twende kutumikia huko Madagaska kwa mwaka mmoja. Tulitaka kwenda, lakini tulikabili vizuizi viwili vikubwa. Baba yangu ambaye alikuwa amezeeka alihitaji kutunzwa, na Veera alikuwa na matatizo ya afya. Nilihuzunika baba yangu alipokufa mnamo Novemba 1990, lakini kwa kuwa Veera alipata nafuu, tulikuwa na tumaini la kurudia kazi ya umishonari. Tulirudi Madagaska mnamo Septemba 1991.
Mgawo wetu huko Madagaska ulikuwa wa mwaka mmoja, lakini uliendelea kwa miaka kumi. Wakati huo, idadi ya wahubiri iliongezeka kutoka 4,000 hadi 11,600. Nilifurahia sana kutumika nikiwa mmishonari. Hata hivyo, wakati mwingine nilivunjika moyo nikifikiria kwamba nilikuwa nikipuuza mahitaji ya kimwili na ya kihisia ya mke wangu mpendwa. Yehova alitupa sote wawili nguvu za kuendelea.
-
-
Tuliazimia Kumtumikia YehovaMnara wa Mlinzi—2006 | Aprili 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 14, 15]
Katika kazi ya mzunguko huko Finland mnamo 1960 . . .
. . . kisha kazi ya umishonari huko Madagaska mnamo 1962
-