Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ugonjwa Ulioogopwa Zaidi Katika Karne ya 19
    Amkeni!—2010 | Oktoba
    • “Hakuna Ugonjwa Mbaya Uliolipuka”

      Katika miaka ya 1970, mateso yaliwafanya Mashahidi wengi wa Yehova waondoke nchini Malawi. Walikimbilia nchi jirani ya Msumbiji, ambako wanaume, wanawake, na watoto zaidi ya 30,000 waliishi katika kambi kumi za wakimbizi. Kama inavyojulikana, mara nyingi magonjwa yanayoenezwa kupitia maji husambaa upesi katika kambi za wakimbizi. Kwa hiyo, Mashahidi waliishi jinsi gani chini ya hali hizo?

      Lemon Kabwazi, pamoja na wengine 17,000 waliishi katika kambi kubwa zaidi huko Mlangeni. Anakumbuka hivi: “Kambi ilikuwa safi kila wakati. Mashimo ya choo yalichimbwa nje ya kambi, na hakuna mtu aliyeruhusiwa ajichimbie shimo lake ndani ya kambi. Vilevile mashimo ya takataka yalichimbwa mbali na kambi. Wajitoleaji walidumisha usafi katika kila njia, kutia ndani kuhakikisha kwamba maji yaliyochotwa katika visima vilivyochimbwa katika eneo tofauti nje ya kambi yalikuwa safi. Ingawa tulikuwa wengi na tuliishi katika eneo dogo sana, tulidumisha viwango vya Biblia kuhusu usafi, kwa hiyo hakuna ugonjwa mbaya uliolipuka, na hakuna mtu aliyewahi kuugua kipindupindu.”

  • Ugonjwa Ulioogopwa Zaidi Katika Karne ya 19
    Amkeni!—2010 | Oktoba
    • [Picha katika ukurasa wa 22]

      Huko Msumbiji, wanaume, wanawake, na watoto zaidi ya 30,000 waliishi katika kambi kumi za wakimbizi ambazo zilidumishwa zikiwa safi

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki