Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Visababishi Vilivyotia Mizizi, Athari Mbaya za Utapiamlo
    Amkeni!—2003 | Februari 22
    • [Sanduku katika ukurasa wa 7]

      JE, MTOTO WAKO ANA UTAPIAMLO?

      Wataalamu wa afya wanawezaje kujua kama mtoto ana utapiamlo? Huenda wakachunguza dalili fulani-fulani, wakauliza maswali kuhusu mazoea yake ya kula, na kuomba apimwe kwenye maabara. Hata hivyo, mara nyingi wao humpima mtoto moja kwa moja. Wao hupima mwili wa mtoto na kulinganisha vipimo hivyo na vipimo vya kawaida. Na hivyo wanajua mtoto anakosa chakula gani na athari za ugonjwa huo.

      Vitu muhimu sana wanavyopima ni uzito, kimo, na unene wa mkono. Wanaweza kujua athari za utapiamlo kwa kulinganisha uzito wa mwili na umri wake; mtoto aliyeathiriwa sana huwa amedhoofika na kukonda. Mtoto huonwa kuwa ameathiriwa sana na utapiamlo iwapo uzito wake umepungua kwa asilimia 40, na ameathiriwa kwa kadiri ikiwa uzito wake umepungua kwa asilimia 25 hadi 40, na ameathiriwa kidogo iwapo uzito wake umepungua kwa asilimia 10 hadi 25. Ikiwa mtoto ana uzito mdogo sana na umri wake ni mkubwa, hiyo ni ishara ya kwamba ni mgonjwa sana—na hakui kamwe.

      Ugonjwa wa marasmus, ugonjwa wa kwashiorkor, na mchanganyiko wa magonjwa hayo mawili husababishwa na aina ya utapiamlo ulio hatari sana wa kukosa vyakula vinavyojenga mwili. Ugonjwa wa marasmus huwapata watoto wanaonyonya wenye umri wa kati ya miezi 6 na miezi 18. Huanza polepole kwa upungufu mkubwa wa nishati, vitamini na madini na husababishwa na kutonyonya vya kutosha au kula vyakula vya badala visivyo na virutubisho vya kutosha. Mtoto mwenye ugonjwa huo hukonda sana, misuli yake hunyauka kiasi cha kubaki mifupa na ngozi, naye hakui. Uso wake huwa kama wa mtu aliyezeeka, anakasirika haraka na kulia sana.

      Neno la Kiafrika kwashiorkor linamaanisha “mtoto aliyeachishwa.” Linawahusu hasa watoto ambao wanaachishwa kunyonya ili ndugu au dada zao wachanga zaidi wanyonye. Ugonjwa huo huanza baada ya mtoto kuachishwa kunyonya. Unasababishwa na ukosefu mkubwa sana wa protini na upungufu wa kalori mwilini. Maji hurundamana mwilini na kumfanya mtoto avimbe tumbo, mikono na miguu. Nyakati nyingine uso wake huvimba na kuwa na umbo la mwezi mpevu. Vidonda hutokea kwenye ngozi na nywele hubadilika rangi na kukauka. Watoto wenye ugonjwa huu huvimba ini, hukosa uchangamfu na furaha. Ndivyo alivyokuwa Erik, aliyetajwa awali, ambaye alinyonyeshwa na mamaye kwa mwezi mmoja tu; kisha akaanza kunyweshwa maziwa ya ng’ombe yaliyotiwa maji. Alianza kunyweshwa mchuzi wa mboga na maji yenye sukari akiwa na umri wa miezi mitatu na kuachiwa jirani amtunze.

      Aina ya tatu ya utapiamlo huwa ni mchanganyiko wa ugonjwa wa marasmus na kwashiorkor. Magonjwa hayo yanaweza kuua yasipotibiwa haraka.

  • Visababishi Vilivyotia Mizizi, Athari Mbaya za Utapiamlo
    Amkeni!—2003 | Februari 22
    • Mtoto hawezi kukua au kusitawi vizuri asipopata vitamini na madini muhimu. Yeye hulia bila sababu yoyote na kuwa mgonjwa-mgonjwa. Kadiri hali yake inavyozorota ndivyo anavyozidi kukonda, macho na utosi wa kichwa hubonyea, ngozi na tishu za mwili hukauka, na uwezo wa kudhibiti joto la mwili hupungua.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki