-
Msiba Mkubwa SanaAmkeni!—2003 | Februari 22
-
-
Ni Nani Wanaopatwa na Ugonjwa Huo?
Utapiamlo hauwapati watoto peke yao. Ripoti ya shirika la WHO ya mwezi wa Julai 2001 inasema kwamba “utapiamlo unasambaa sana, unawaathiri watu wapatao milioni 800—asilimia 20 ya watu wanaoishi katika nchi zinazoendelea.” Hiyo yamaanisha kwamba mtu 1 kati ya kila watu 8 ulimwenguni ana utapiamlo.
Ingawa idadi kubwa ya watu wasiopata chakula cha kutosha wako Asia—hasa kwenye maeneo ya kusini na ya kati—bara la Afrika lina idadi kubwa zaidi ya watu wasiopata chakula cha kutosha ukilinganisha na idadi ya watu wanaoishi humo. Kisha inafuatwa na nchi kadhaa zinazoendelea za Amerika ya Latini na Karibea.
Je, nchi zilizoendelea zinakumbwa na ugonjwa huo? Ndiyo. Kichapo The State of Food Insecurity in the World 2001 kinasema kwamba watu milioni 11 wanaoishi katika nchi zilizoendelea wana utapiamlo. Na watu wengine milioni 27 walio na utapiamlo wanaishi katika nchi zinazoendelea kusitawi kiviwanda, hasa nchi zilizo Mashariki mwa Ulaya na jamhuri za ule uliokuwa Muungano wa Sovieti.
-
-
Msiba Mkubwa SanaAmkeni!—2003 | Februari 22
-
-
[Chati/Ramani katika ukurasa wa 4]
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
NCHI ZINAZOKABILI UHABA WA CHAKULA BORA
UHABA MKUBWA
UHABA WA WASTANI
UHABA MDOGO
HAKUNA UHABA AU TAKWIMU KAMILI HAZIPATIKANI
-