-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
“Utando wa sehemu ya mbele ya bongo kubwa . . . huhusika sana katika kuchanganua kabisa mawazo, akili, kichocheo, na utu. Sehemu hiyo hushirikisha mambo yanayoonwa maishani ambayo ni muhimu katika kufikiria mambo, kufanya uamuzi, kuwa mwenye udumifu, kupangia mambo, kuwahangaikia wengine, na dhamiri. . . . Uchanganuzi wa habari katika sehemu hii ndio huwafanya wanadamu wawe tofauti na wanyama wengine.” (Human Anatomy and Physiology cha Marieb) Kwa kweli twaona uthibitisho wa tofauti hii kati ya wanadamu na wanyama kwa kutazama matimizo ya mwanadamu katika mambo kama hesabu, falsafa, na haki, mambo ambayo kwa msingi hutegemea utando wa sehemu ya mbele ya bongo kubwa.
Kwa nini wanadamu wana utando mkubwa wa sehemu ya mbele ya bongo kubwa, ambao ni wenye kubadilikana, na ambao huchangia sana kufikiri kwa hali ya juu, ilhali katika wanyama sehemu hiyo ni ndogo sana au hata haipo kabisa? Tofauti hiyo ni kubwa sana hivi kwamba wanabiolojia wanaosema kwamba sisi tumetokea kupitia mageuzi husema juu ya “ukuzi mkubwa sana wa ghafula wa ubongo wa binadamu.” Profesa wa Biolojia Richard F. Thompson, akisema juu ya ukubwa usio wa kawaida wa utando wa bongo kubwa wa binadamu, akiri hivi: “Kufikia sasa hatuelewi kabisa ni kwa nini jambo hili lilitukia.” Je, inawezekana sababu ni kwamba mwanadamu aliumbwa akiwa na ubongo wenye uwezo mkubwa usio na kifani?
-
-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 54]
“Karibu ubongo wote wa binadamu umefanyizwa na utando [wa bongo kubwa]. Kwa mfano, ubongo wa sokwe una utando pia, lakini ni mdogo sana kwa kulinganishwa. Huo utando hutuwezesha kufikiri, kukumbuka, na kuwazia mambo. Kwa msingi, sisi ni binadamu kwa sababu ya utando wetu.”—Edoardo Boncinelli, mkurugenzi wa utafiti wa biolojia ya molekuli, Milan, Italia.
-
-
Jinsi Ulivyo Kiumbe cha Kipekee!Je, Kuna Muumba Anayekujali?
-
-
●Utando wa Bongo Kubwa ndio utando wa nje wa bongo unaohusika sana na akili. Utando wa bongo kubwa wa binadamu ukilainishwa unaweza kufunika kurasa nne; wa sokwe unaweza kufunika ukurasa mmoja tu; na wa panya unaweza kufunika stampu ya barua.—Scientific American.
-