-
Vitabu vya Injili Vinategemeka Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
Watu haohao wamekata kauli kwamba Marko ndiye aliyeandika kitabu cha kwanza cha Injili, kwa kuwa anaongezea habari chache kwa vitabu vya Mathayo na Luka. Pia wachambuzi hao wamedai kwamba Mathayo na Luka walitumia kitabu cha Marko kuandika vitabu vyao na kwamba walitumia hati ya ziada iliyoitwa na wasomi Q (herufi inayotokana na neno la Kijerumani Quelle, au “chanzo”).
-
-
Vitabu vya Injili Vinategemeka Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
Je, Injili ya Marko Iliandikwa Kwanza?
Wazo la kwamba Injili ya Marko iliandikwa kwanza na kwamba ilitumiwa na Mathayo na Luka halina “msingi hakika,” inasema kamusi moja ya Biblia (The Anchor Bible Dictionary). Hata hivyo, wasomi wengi wanaamini kwamba Marko aliandika Injili yake kabla ya Mathayo na Luka kwa sababu wanadai kwamba Marko hakuandika mambo mengi ya ziada kuliko Injili nyingine. Kwa mfano, msomi wa Biblia wa karne ya 19 Johannes Kuhn alisisitiza kwamba ni lazima Injili ya Marko iwe iliandikwa kwanza. La sivyo, Kuhn alisema, “mtu angehitaji kufikiri kwamba Marko alikata Injili ya Mathayo na Luka katika vipande vidogo-vidogo na kuvichanganya kwenye nyungu na kutokeza Injili kutokana na mchanganyiko huo.”
Kwa kuwa Injili ya Marko ndiyo fupi zaidi, haishangazi kwamba ina habari chache za pekee. Hata hivyo, hilo halithibitishi kwamba ni lazima iwe iliandikwa kwanza. Zaidi ya hilo, si kweli kwamba Marko haandiki mambo yoyote ya ziada kuliko yale yaliyo katika Injili ya Mathayo na Luka. Katika simulizi linaloambatanisha kwa haraka matukio ya huduma ya Yesu kuna habari zenye kupendeza na mistari zaidi ya 180 ambayo haipatikani katika Mathayo na Luka, hivyo kulifanya kuwa simulizi la pekee la maisha ya Yesu.—Ona sanduku kwenye ukurasa wa 13.
-
-
Vitabu vya Injili Vinategemeka Kadiri Gani?Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 1
-
-
Ushuhuda wa waandikaji wa kale wa mafundisho ya Kikristo kutia ndani mwanatheolojia Origen, unaonyesha pia kwamba mtume Mathayo ndiye aliyekuwa wa kwanza kuandika kitabu cha Injili. Origen aliandika hivi: “Kitabu cha kwanza kiliandikwa na Mathayo, aliyekuwa mkusanya-kodi, lakini baadaye akawa mtume wa Yesu Kristo, alikiandika katika Kiebrania kwa ajili ya Wayahudi waliogeuzwa imani.” Ni wazi kwamba mtume Mathayo aliyekuwapo mambo aliyoandika yalipotukia hakuhitaji kuiba maandishi ya Marko ambaye hakujionea matukio hayo.
-