-
Marko ‘Mwenye Faida kwa Ajili ya Huduma’Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
Walipatana
Bila shaka, jambo hilo lilimhuzunisha sana Marko. Hata hivyo, aliendelea kuwa mhudumu mwaminifu. Miaka 11 au 12 hivi baada ya kukosana na Paulo, Marko anatajwa tena katika utendaji wa Wakristo wa mapema. Akiwa na nani? Akiwa na mtu ambaye hungetazamia kamwe, Paulo!
Katika mwaka wa 60-61 W.K., Paulo alipokuwa gerezani huko Roma, alituma barua fulani ambazo sasa ni sehemu ya Maandiko Matakatifu. Katika barua kwa Wakolosai, aliandika hivi: “Aristarko mateka mwenzangu anawatumia ninyi salamu zake, na pia Marko binamu ya Barnaba, (ambaye mlipokea amri kumhusu yeye ili mkamkaribishe ikiwa atakuja kwenu) . . . Ni hawa tu walio wafanyakazi wenzangu kwa ajili ya ufalme wa Mungu, na hawa ndio wamekuwa msaada wenye kunitia nguvu.”—Kol. 4:10, 11.
Hilo lilikuwa badiliko kubwa kama nini! Mwanzoni Marko alimkasirisha sana Paulo, lakini sasa Paulo alimthamini sana akiwa mfanyakazi mwenzake. Inaonekana Paulo aliwajulisha Wakolosai kwamba huenda Marko angewatembelea. Ikiwa Marko angewatembelea, angekuwa mwakilishi wa Paulo.
Je, inawezekana kwamba Paulo alimchambua Marko kupita kiasi miaka iliyotangulia? Je, Marko alifaidika na nidhamu aliyopata? Au labda mambo hayo mawili yalihusika? Vyovyote vile, Paulo na Marko walionyesha kwamba walikuwa wakomavu kwa sababu walipatana tena. Walisahau jambo lililotukia kati yao zamani nao wakatumika tena pamoja. Ni mfano mzuri kama nini kwa mtu yeyote ambaye amekosana na Mkristo mwenzake!
-
-
Marko ‘Mwenye Faida kwa Ajili ya Huduma’Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
Paulo alipofungwa gerezani kwa mara ya pili huko Roma karibu mwaka wa 65 W.K., alimwandikia Timotheo huko Efeso na kuongezea hivi: “Umchukue Marko na uje pamoja naye.” (2 Tim. 4:11) Kwa hiyo, wakati huo Marko alikuwa Efeso. Hatuna shaka yoyote kwamba alikubali ombi la Paulo la kurudi Roma pamoja na Timotheo. Safari zilikuwa ngumu wakati huo, lakini Marko alifunga safari hizo kwa kupenda.
-
-
Marko ‘Mwenye Faida kwa Ajili ya Huduma’Mnara wa Mlinzi—2010 | Machi 15
-
-
“Mwenye Faida Kwangu kwa Ajili ya Huduma”
Zaidi ya kuandika Injili yake, Marko alifanya mambo mengine huko Roma. Kumbuka maneno ambayo Paulo alimwambia Timotheo: “Umchukue Marko na uje pamoja naye.” Kwa nini Paulo alisema hivyo? “Kwa maana yeye ni mwenye faida kwangu kwa ajili ya huduma.”—2 Tim. 4:11.
Uhakika wa kwamba Marko anatajwa katika vitabu vya Maandiko vilivyoandikwa mwisho unafunua mengi kumhusu. Katika masimulizi yote kuhusu utendaji wake kutanikoni, Marko hatajwi popote kuwa mtume, kiongozi, au nabii. Alikuwa mhudumu, yaani, aliwahudumia na kuwatumikia wengine. Na muda mfupi kabla ya kifo cha Paulo, bila shaka Marko alimsaidia sana mtume huyo.
-