-
Marko Hakukata TamaaMnara wa Mlinzi—2008 | Februari 1
-
-
Mwaka wa 47 W.K., Barnaba na Sauli walichaguliwa wafanye kazi ya umishonari. Walimchukua Marko kwenda pamoja nao, lakini kwa sababu fulani zisizoelezwa, baadaye Marko aliwaacha na kurudi nyumbani, Yerusalemu. Sauli, aliyejulikana baadaye kwa jina lake la Kiroma Paulo, alikasirika. Na hakupuuza ule ambao aliona kuwa udhaifu mkubwa wa Marko.—Matendo 13:1-3, 9, 13.
Waliporudi kutoka safari yao ya umishonari, Paulo na Barnaba walieleza mafanikio mazuri sana ambayo walipata. (Matendo 14:24-28) Miezi mingi baadaye, wanaume hao wawili walipanga kurudi na kuwatembelea wanafunzi wapya katika maeneo ambako walikuwa wamehubiri. Barnaba alitaka waende pamoja na Marko, lakini je, unajua Paulo alikuwa na maoni gani?— “Hakuona kwamba inafaa” kwa sababu mapema Marko aliwaacha na kurudi nyumbani.
-
-
Marko Hakukata TamaaMnara wa Mlinzi—2008 | Februari 1
-
-
Baadaye, Paulo alipokuwa gerezani huko Roma, alimpongeza Marko kwa kumsaidia kwa ushikamanifu. (Wakolosai 4:10, 11) Na Paulo alipokuwa tena gerezani huko Roma, alimwandikia Timotheo na kumwomba amlete Marko, na akaeleza hivi: “Yeye ni mwenye faida kwangu kwa ajili ya huduma.” (2 Timotheo 4:11) Kwa kweli, Marko alipata mapendeleo makubwa kama nini ya utumishi kwa sababu hakukata tamaa!
Marko alipata baraka gani kwa kutokata tamaa?
-