-
Tahiti2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Wamishonari wa Mwisho Wafika
Wamishonari wa mwisho kufika kutoka Ufaransa ni Serge na Marie-Louise Gollin, waliofika Novemba 1990. Wao pia walitumwa Marquesas, ambako wamesaidia sana kuimarisha makutaniko. Ndugu na Dada Gollin wamejifunza lugha ya Marquesas, na jambo la kuvutia ni kwamba wametembelea kila jamaa kwenye visiwa sita vinavyokaliwa!
Ndugu na Dada Gollin wanaishi kwenye kisiwa cha Hiva Oa, ambako hakuna mzee mwingine isipokuwa Serge. Wanahubiri kwa ukawaida kwenye visiwa kadhaa, kutia ndani visiwa viwili visivyo na wahubiri. Walipotembelea kisiwa cha Fatu Hiva kwa mara ya kwanza, Serge alishangaa kwamba mashemasi wa Kanisa Katoliki na Kanisa la Kiprotestanti waliwaunga mkono. Baada ya ibada katika makanisa yao, mashemasi hao waliwaalika watu wasikilize hotuba ya watu wote ya nusu saa ambayo Serge alitoa kwa kawaida kwenye shule ya eneo hilo. Isitoshe, shemasi wa Kanisa la Kiprotestanti alitafsiri hotuba ya Serge katika lugha ya Marquesasas, kwa kuwa wakati huo aliijua lugha hiyo vizuri kuliko Serge.
Ili kuwasaidia wasikilizaji wapate maandiko katika Biblia zao, Serge aliyaandika kwenye ubao. Pia alitoa sala, na wote wakasema “Amina.” Kesho yake, Ndugu na Dada Gollin waliiachia kila familia kwenye kisiwa cha Fatu Hiva vitabu. Tangu wakati huo, wamekaribishwa kwa uchangamfu kila wanapotembelea kisiwa hicho chenye watu 600 hivi.
-
-
Tahiti2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 120]
Marie-Louise na Serge Gollin ni mishonari huko Marquesas
-