Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tahiti
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ili kuwasaidia wamishonari hao wawili, ofisi ya tawi iliwatuma mapainia wa pekee kutoka Tahiti kuhubiri pamoja nao. Mmoja wao ni Pascal Pater, ambaye sasa ni mzee wa kutaniko na yule mwingine ni Michel Bustamante, ambaye sasa ni mwangalizi wa mzunguko. Vijana hao wenye bidii walifurahi kutumia nguvu zao za ujana kumtumikia Yehova. (Met. 20:29) Na bila shaka walihitaji nguvu, kwa kuwa mtu dhaifu au mwoga hangefaulu kuhubiri kwenye Visiwa vya Marquesas. Hakukuwa na barabara. Ili kufika kwenye nyumba na vijiji vya mbali, walisafiri kwenye vijia vyenye mawe na vya matope na kwenye mabonde, katikati ya milima mirefu. Baadhi ya sehemu hizo zilifikika tu kwa kutumia pikipiki ndogo.

  • Tahiti
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Michel Bustamante anasema: “Utumishi wangu kwenye visiwa hivyo ulikuwa wenye kusisimua na wenye kuvutia. Lakini tulipatwa na mambo yenye kutisha pia, hasa tulipokuwa peke yetu kwenye visiwa fulani. Pindi moja nilikaa katika nyumba iliyokuwa kwenye bonde lenye giza-giza, mbali na mahali nilipokuwa nimehubiri siku hiyo. Nilitafuta mahali pa kulala katika kijiji kilichokuwa karibu, lakini sikufaulu, kwa hiyo ikanibidi kurudi nyumbani. Giza lilikuwa limeingia na miamba mirefu ilionekana kuwa yenye kuogofya sana usiku. Nilianza kufikiria uchawi wa eneo hilo, na mashetani ambao bila shaka walisambaa kotekote. Kwa sababu ya woga, nilianza kusali na kuimba nyimbo za Ufalme zinazotaja jina la Yehova mara nyingi. Nilipoingia nyumbani kwangu hatimaye, nilifunga mlango, nikafungua Biblia, na kuanza kusoma. Polepole nilianza kujihisi salama.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki