Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Ndoa Yenye Matatizo
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
    • 4 Baadhi ya Wakristo hawaoi au kuolewa “katika Bwana tu” na hivyo wanateseka sana kwa sababu ya kuwa katika familia iliyogawanyika kidini. (1 Kor. 7:39) Ikiwa unapitia hali hiyo, sali ili Mungu akusamehe na kukusaidia. Mungu haondoi madhara yanayosababishwa na makosa ambayo mtu alifanya zamani, lakini anawasaidia wale wanaotubu kuvumilia majaribu. (Zab. 130:1-4) Jitahidi kwa moyo wote kumpendeza sasa na milele, na ‘shangwe ya Yehova itakuwa ngome yako.’—Neh. 8:10.

  • Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Ndoa Yenye Matatizo
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
    • Fikiria jambo linaloweza kutokea katika familia iliyogawanyika kidini. Mtume Petro aliandika hivi: “Ninyi wake, jitiisheni kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu kwa lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa wake zao, kwa sababu wamekwisha kushuhudia kwa macho mwenendo wenu ulio safi kiadili pamoja na heshima kubwa.” (1 Pet. 3:1, 2) Naam, mwenzi ambaye si mwamini anaweza kukubali kweli kwa sababu ya mwenendo mzuri wa mwenzi wake mwamini! Ndoa hiyo ambayo imeokolewa inamletea Mungu heshima na inaweza kumletea baraka nyingi mume, mke, na watoto ambao huenda wakawa nao.

  • Uwe na Maoni Yanayofaa Kuhusu Ndoa Yenye Matatizo
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Mei 15
    • 13. Ni shauri gani linalopatikana katika 1 Wakorintho 7:10-16?

      13 Wazee wanapoombwa wawasaidie Wakristo wanaoishi katika familia iliyogawanyika kidini, wanarejelea shauri kama la Paulo, aliyeandika hivi: “Kwa watu waliofunga ndoa natoa maagizo, lakini si mimi bali ni Bwana, kwamba mke hapaswi kuondoka kwa mume wake; lakini kwa kweli akiondoka, na akae mseja kama sivyo apatane tena na mume wake; na mume hapaswi kumwacha mke wake. . . . Kwa maana, wewe mke, unajuaje kama utamwokoa mume wako? Au, wewe mume, unajuaje kama utamwokoa mke wako?” (1 Kor. 7:10-16) Inakuwa baraka kama nini wakati mwenzi wa ndoa ambaye si mwamini anapovutiwa  na kujiunga na ibada ya kweli!

      14, 15. Ni wakati gani kwa kweli mwenzi wa ndoa Mkristo anaweza kufikiria kuondoka, lakini kwa nini ni muhimu asali kuhusu jambo hilo na kulifikiria kwa unyoofu?

      14 Ni katika hali gani mke Mkristo anaweza ‘kwa kweli kuondoka’? Wengine wameamua kutengana kwa sababu mwenzi wao anakataa kimakusudi kuandaa mahitaji ya familia. Wengine wametengana kwa sababu mwenzi wao anawatesa sana kimwili au anahatarisha kabisa hali yao ya kiroho wakiwa Wakristo.

      15 Kutengana au kutotengana na mwenzi wa ndoa ni uamuzi wa mtu binafsi. Hata hivyo, mwenzi aliyebatizwa anapaswa kusali kuhusu jambo hilo na kulifikiria kwa unyoofu. Kwa mfano, je, mwenzi ambaye si mwamini ndiye ambaye amehatarisha kabisa hali ya kiroho ya mwenzi Mkristo, au je, Mkristo mwenyewe amekuwa akipuuza funzo la Biblia, amekuwa hahudhurii mikutano kwa ukawaida, na hashiriki kwa ukawaida katika huduma?

      16. Ni nini kinachopaswa kuwazuia Wakristo kuamua haraka-haraka kutalikiana?

      16 Uhakika wa kwamba tunathamini uhusiano wetu pamoja na Mungu na kuthamini zawadi yake ya ndoa unapaswa kutuzuia kuamua haraka-haraka kutalikiana. Tukiwa watumishi wa Yehova, tunahangaikia kutakaswa kwa jina lake takatifu. Basi, bila shaka hatungetaka kamwe kupanga njama ya kumwacha mwenzi wetu wa ndoa huku tukipanga moyoni kuoa au kuolewa na mtu mwingine.—Yer. 17:9; Mal. 2:13-16.

      17. Ni katika hali gani inaweza kusemwa kwamba Mungu amewaita Wakristo waliofunga ndoa kwenye amani?

      17 Mkristo ambaye ameoa au kuolewa na mtu ambaye si mwamini anapaswa kujitahidi kabisa kuendelea kudumisha kifungo cha ndoa. Hata hivyo, Mkristo hahitaji kujiona kuwa na hatia ikiwa amejitahidi kwa unyoofu kudumisha kifungo cha ndoa lakini mwenzi wake wa ndoa ambaye si mwamini anakataa kuendelea kuishi naye. Paulo aliandika hivi: “Yule asiyeamini akiondoka, acha aondoke; ndugu au dada hayumo katika utumwa chini ya hali za namna hiyo, lakini Mungu amewaita ninyi kwenye amani.”—1 Kor. 7:15.b

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki