Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Ndoa Inaweza Kustahimili Msukosuko?
    Amkeni!—2006 | Julai
    • Ndoa Yashambuliwa

      Ndoa imekuwa ikishambuliwa tangu mwanzo wa historia ya wanadamu. Sifa na mitazamo iliyokuzwa na wazazi wetu wa kwanza imetokeza msukosuko tunaoona leo katika ndoa. Adamu na Hawa walifanya dhambi walipojiruhusu washindwe na tamaa za kibinafsi na hivyo ‘dhambi ikaingia katika ulimwengu.’ (Waroma 5:12) Rekodi ya historia ya Biblia inasema kwamba punde baada ya hapo, “kila mwelekeo wa fikira za moyo [wa mwanadamu] ulikuwa mbaya tu wakati wote.”—Mwanzo 6:5.

      Hali haijabadilika sana tangu wakati huo. Kati ya maelekeo yenye kudhuru ambayo yanakabili ndoa ni kujaribu kujitosheleza bila kujizuia. Huenda mpango wa ndoa ukaonekana kuwa umepitwa na wakati na kwamba haufai katika ulimwengu wa kisasa unaoongozwa na maadili mapya. Na kulegezwa kwa sheria ambazo huzuia kuvunjika kwa ndoa kumeondoa aibu ambayo hapo awali ilihusianishwa na talaka.

      Watu wasio na subira ambao hutaka kujitosheleza mara moja, hawafikirii sana au hawafikirii hata kidogo kuhusu madhara ya talaka. Wakidhani kwamba watapata uhuru, wanaamini kuwa talaka italeta furaha.

      Watu fulani wanapokabili matatizo magumu katika ndoa, wao hutafuta msaada wa washauri wa ndoa au vitabu vilivyoandikwa na watu hao. Kwa kusikitisha, baadhi ya “wataalamu” wa ndoa wa kisasa wamekuwa wakichochea talaka badala ya kutetea ndoa. Kitabu The Case for Marriage kinasema kwamba “labda kwa mara ya kwanza katika historia ya wanadamu, ndoa, mpango ambao umeheshimiwa kwa muda mrefu, inazidi kushambuliwa kwa mafanikio. Nyakati nyingine ndoa hushambuliwa moja kwa moja na ‘wataalamu’ wanaoamini kwamba ni jambo lenye kukandamiza au lisilopatana na akili kuweka nadhiri ya kuishi pamoja muda wote wa maisha.”

      Maoni ya Watu Yamebadilika

      Pia maoni ya watu kuhusu ndoa na kusudi la ndoa yamebadilika. Labda umeona kwamba watu hawaoni umuhimu wa wenzi wa ndoa kuwa waaminifu na kutegemezana. Jambo kuu kwao ni kujitosheleza hata ikiwa mara nyingi kufanya hivyo kutamuumiza mwenzi yule mwingine. Jarida Journal of Marriage and Family linasema kwamba badiliko hilo la maoni ya ubinafsi kuhusu ndoa “lilianza katika miaka ya 1960 na kuongezeka haraka katika miaka ya 1970.” Sababu za msingi ambazo ziliwafanya watu wafunge ndoa, kama vile kutamani kupendwa, kuwa na uhusiano wa karibu, uaminifu, watoto, na kutoshelezana, hazionwi kuwa muhimu sana.

      Matukio mengine ya hivi karibuni yamechangia sana kubadilika kwa ndoa katika nchi nyingi. Kwanza, katika nchi nyingi, majukumu ya mwanamume ya kutafuta riziki na ya mwanamke ya kutunza nyumba yamebadilika. Kwa kuwa wanawake wameanza kufanya kazi za kuajiriwa, kumekuwa na ongezeko la familia ambazo waume na wake hufanya kazi. Pili, kupata watoto nje ya ndoa ni jambo linalozidi kukubaliwa, hivyo kuongeza idadi ya familia zenye mzazi mmoja. Tatu, watu wengi zaidi wanaishi pamoja bila kufunga ndoa. (Ona sanduku “Si Thabiti Kama Ndoa.”) Nne, ndoa kati ya watu wa jinsia moja na harakati zinazotetea kuhalalishwa kwa ndoa hizo zimeungwa mkono na watu wengi. Je, matukio hayo ya kisasa yameathiri maoni yako kuhusu ndoa?

  • Je, Ndoa Inaweza Kustahimili Msukosuko?
    Amkeni!—2006 | Julai
    • [Blabu katika ukurasa wa 5]

      “Katika jamii ambayo imezoea kutupa vitu, huenda watu wakawa na mtazamo huohuo kuhusu mahusiano.”—SANDRA DAVIS, MTAALAMU WA SHERIA YA FAMILIA

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki