-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Kielelezo cha Ndoa ya Hali ya Juu
Watu wanapofunga ndoa, kila mmoja wao hutazamia mambo fulani katika muungano huo wa ndoa. Lakini Mungu ana matazamio gani? Ni yeye aliyeanzisha muungano wa ndoa. Alikusudia iwe namna gani?
Jambo moja la kuonyesha maoni ya Mungu kuhusu ndoa linatokana na uhusiano wake na taifa la Israeli katika mambo mbalimbali. Isaya anauonyesha uhusiano huo kuwa kama ndoa. (Isaya 62:1-5) Angalia mambo ambayo Yehova Mungu akiwa kama “mume” anamfanyia “bibi-arusi” wake. Anamlinda na kumtakasa. (Isaya 62:6, 7, 12) Anamheshimu na kumthamini. (Isaya 62:3, 8, 9) Na anamfurahia sana huyo mke, kama vile inavyoonyeshwa na majina mapya anayompa.—Isaya 62:4, 5, 12.
-
-
“Jina Jipya”Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hakuwezi kuwako upendo mkubwa kuliko ule ulioonyeshwa na Yehova kuelekea Israeli na ule unaoonyeshwa na Kristo kuelekea kutaniko. Visa hivyo vya uhusiano wa kimfano vinaandaa kielelezo cha ndoa ya hali ya juu, yenye mafanikio na furaha kati ya Wakristo.—Waefeso 5:28-33.
-